Msaada- Nimetapeliwa Kariakoo- Vitasa 100 feki za milango sawa na TSH 2.3million

Msaada- Nimetapeliwa Kariakoo- Vitasa 100 feki za milango sawa na TSH 2.3million

Nenda ubungo plazza kaulize FCC,fair competition commission,ina fanya kazi na ku mtetea mraji,mi niliuziwa flash feki mwaka 2012,nilienda tbs,tbs wakaniambia niende hapo,nilipoenda wakanipa barua niwapeleke walioniuzia flash fake ikisema wanipe hela au wanibadilishie,wakanikatalia kurudisha hela hata kubadilisha,nikaenda kutoa taarifa tena,ndipo nikaondoka nao kutumia gali lao hadi kariaokoo,kufika pale wakaawaambia either wanipe hela yangu au watoe faini milioni mbili,wale jamaa wakaamua kunirudishia hela yangu yote.
kama upo serious fanya hivyo,wewe nenda pale ubungo plaza kaulizie ofisi za fair competiton,watakusaidia,walikuwa hawanijui,wala siwajui,ila walinisaidia kupata haki yangu.
 
Salaam wana Jamvi,
Katika hali ya kushangaza, picha hapo chini ni kitasa chamlango wangu nilionunua wiki 2 zilizopita. Kariakoo, risiti ninazo (TZS 100@230,000=2.3million). Cha kushangaza ni kwambazinasambaratikavyenyewe(bila kugongwa). Cha kushangaza niliporudikwa muuzaji badala ya kunionea huruma, ananiambia risiti imeandikwa maliikishauzwa hairudishwi, ilibidi niwe mpole kama mama lishe!!
Msaada: Naombeni msaada sehemu muafaka/dukana aina ya kitasa imara nay a kudumu kabisa, hata kama ni expensive siyoissue(quality speaks better than quantity).

Mkuu umeandika kama unakimbizwa? M nmeelewa vitasa umetapeliwa, sasa unata urudishiwe fedha japo rist imeandikwa hairudishwi mali aliyo nunua au mahali pa kupata vitasa?

Nextime, usiende mwenyewe kununua mpe fundi anaekujengea utapata vitasa vyema.. Au nenda mliman city hapo utapta mpaka warrant,

Pole kwa kupigwa hyo ndo bongo, ww umelia wenzio wamecheka, haya maisha bwana yaache tuuuu..
 
Mkuu Nchi hii ni yetu sote! Uozo kama huu lazima tufike mahali kuuondoa kama si kuumaliza lakini hata kuupunguza.
TSh 2 .3ml ni pesa nyingi kupotea hivi hivi kwenye bidhaa feki.Tafadhali peleka Bidhaa hiyo feki TBS na Chama cha walaji ilikuepusha kuumizwa kwa mtu mwingine huu mtandao wa bidhaa feki wananeemeka na kupata utajiri wa haraka.



NB. Mkuu Invisible kwa hisani yako naomba kuwasilisha ombi usaidie MODS kufikisha Maombi ili kama inawezekana hawa jamaa wa TBS wakawepo humu JF ili mambo kama haya tupate mahali pakusemea pengine itasaidia Jamii.

Uelewa wa consumer protection hapa kwetu upo chini sana sana. Wanasheria nao sio wabunifu kupanua wigo wa aina za mashauri wanayochukua, hawatoi ushaurikwa wananchi kuwa wana haki kama hawapati huduma muafaka kwa hela wanayolipa. Mifano michache ni kama insurance claims ukiangalia kwa kina utakuta wanaolipwa ni wachache na hao wanaolipwa kiasi ni kidogo sana kulingana na maumivu wanayoyapata.

Kila siku tunanuna airtime ni wachache sana mingoni mwetu twaweza kuthibitisha kuwa kiasi walichotumia ndicho walicholipia. We dont question and kife goes on and the kampuni za simu get richer and richer.

Tunanunua umeme in advance halafu provider anakupa umeme anavyotaka yeye, kwa nini iwe hivyo akichukua hela yake ni LAZIMA AKUPE UMEME asiseme kuna mgao.

Unanunua bia baa kwa bei ya 500 ml unaambiwa hawana na badala yake wanakupa ya 300 ml ukinywa bia tano za 300 ml na ukiwa unapigwa kihivyo utakuwa umepunjwa bia 2 za 500mls and we dont complain.

Mifano ni mingi sana haina mwisho. Something has to be done.
 
Last edited by a moderator:
Nenda pale mwenge itv, asa abloy, wanauza vitasa vya union, hao ndo wakala wa union
 
Hivi inakuwaje mkishapigwa na mnakuja kuweka post?ilikuwa na kizuizi gani kabla ya kununua ungeweka post kuwa unatafuta vitasa?kuna wana jamvi humu wana maduka na wangekushauri aina bora ya vitasa na sio "bora vitasa" Pole lkn kwa ushauri nenda polisi kuna sharia inayoruhusu kurudisha mali dukani baada ya kununua hizo risiti zao na longo longo wala lisikutishe

Ushauri wa kwenda Polisi ni mzuri kabisa. Lakini ushauri wa kuuliza kwanza jamvini ni mgumu. Tutauliza vingapi na mara ngapi? Kuna uhakika gani utapata ushauri mzuri?
 
Kuna sheria zinazokulinda na hali kama hiyo Tanzania, kuna mwanasheria alianzisha "Tanzania Consumer Advocacy Society", fata hii blog na jaribu kuwasiliana nae utapata ufumbuzi, huyo mwenye duka atakulipa gharama zako zote, za usafiri, uchukuzi, ununuzi, ufundi, muda na hasara zilizokupata kwa kukuuzia vitu vibovu, na si za ununuzi tu:

TANZANIA CONSUMER ADVOCACY SOCIETY

Nchi za nje mawakili huwa wanazinunua kesi namna hii huku wanashangilia, nashangaa hapa Tanzania mawakili wetu hamchangamkii ulaji wa uhakika huu.

Naona kama hesabu yako umekosea hapo, hebu rekebisha.

Faiza hii society kama ipo basi vision yao ni ya kizamani sana hawajitangazi yaelekea ni watu wa ofisini na mitandao hawaendi field ambako ndipo uonevu ulipo.

Hata hivyonimwanzo mzuri.
 
Salaam wana Jamvi,
Katika hali ya kushangaza, picha hapo chini ni kitasa chamlango wangu nilionunua wiki 2 zilizopita. Kariakoo, risiti ninazo (TZS 100@230,000=2.3million). Cha kushangaza ni kwambazinasambaratikavyenyewe(bila kugongwa). Cha kushangaza niliporudikwa muuzaji badala ya kunionea huruma, ananiambia risiti imeandikwa maliikishauzwa hairudishwi, ilibidi niwe mpole kama mama lishe!!
Msaada: Naombeni msaada sehemu muafaka/dukana aina ya kitasa imara nay a kudumu kabisa, hata kama ni expensive siyoissue(quality speaks better than quantity).

Dah, pole mkuu. Mara zote unaponunua ulizia guarantee, manufacturer wengi ambao ni legit wanasimamia bidhaa yao hata 2yrs, na hiyo guarantee iwe imeandikwa na terms zake ziwe wazi. Ukiangalia brands peke yake bado utalia kwa sababu hawa matapeli wanaojiita wafanyabiashara wanakwenda china na kuclone brands maarufu. Na huyo usimwache, nenda TBS karipoti na ufuatilie, nadhani kuna mamlaka nyingine inayotetea walaji lakini sikumbuki ni mamlaka gani, hakikisha unafuatilia suala hilo, not only for the 2M, lakini kwa ajili ya kupata haki kwa mujibu wa sheria.
 
Cheap has always been expensive!!!!!

You must be joking 230,000tsh per pc = 143Us Dollar (Rate of 1600tsh) and you still call Cheap ! Anway human being have different income levels but aleast for average Tanzanian for this price you expect better quality.
 
Hapa ndipo ninaposhauri watu wajifunze kutumia vitu vyenye nja kali...Mrudishie mali kabla hujamwambia chochote chomoa hii kitu..
Man-Holding-Gun-1.jpg
 
kaka wasikukutishe tamaa baadhi ya watu humu. Amka nenda TBS watakusaidia ukiona wanalongolongo nyingi ujue wana issue nayo hilo duka. usichoke nenda karipoti police ili hatua za kisheria zianze za kulinda usalama wako kwanza then nenda ukafungue kesi ya madai mahakamani utalipwa pesa yako na fidia juu. Chonde chonde kaka usikae kimya wasaidie wengine wapo wengi sana wanaoliwa lakini hawasemi pia ebu saidia jamii kuonesha tumechoshwa na bidhaa feki.
 
You must be joking 230,000tsh per pcs = 143Us Dollar (Rate of 1600tsh) and you still call Cheap ! Anway human being have different income levels but aleast for average Tanzanian for this price you expect better quality.

"Cheap" in this aspect doest not necessarily mean "Many digits" rather it implies "easily available"


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Faiza hii society kama ipo basi vision yao ni ya kizamani sana hawajitangazi yaelekea ni watu wa ofisini na mitandao hawaendi field ambako ndipo uonevu ulipo.

Hata hivyonimwanzo mzuri.

Wangekuwa hawajitangazi mimi ningewajuwa?

Hao ni watu binafsi waliojitolea, kawasome, nimeweka link ya blog yao, na ukiweza na wewe unaweza kuwatangaza kwa faida yako na wengine kama nilivyofanya mimi.

Msingoje kila kitu kufanyiwa.
 
Wangekuwa hawajitangazi mimi ningewajuwa?

Hao ni watu binafsi waliojitolea, kawasome, nimeweka link ya blog yao, na ukiweza na wewe unaweza kuwatangaza kwa faida yako na wengine kama nilivyofanya mimi.

Msingoje kila kitu kufanyiwa.

Wewe ni kati ya wachache unaowafahamu, wengi waliobaki hawawafahamu na kufanya iwe ngumu kupeleka malalamiko yao.

Ofisi zao ziko wapi ili tusaidie kuwatangaza, maana kwenye blog yao hawaoneshi wanapatikanaje.
 
Wewe ni kati ya wachache unaowafahamu, wengi waliobaki hawawafahamu na kufanya iwe ngumu kupeleka malalamiko yao.

Ofisi zao ziko wapi ili tusaidie kuwatangaza, maana kwenye blog yao hawaoneshi wanapatikanaje.

Fata blog na waandikie, au unaweza pia kutumia google kuwatafuta au unaweza kwenda BRELA ukapata habari zao zote kwani wamejiandikisha rasmi kama wanavyoeleza kwenye blog yao, kwani kwa sasa na wewe umeshawajuwa kuwa wapo.

Usingojee kila kitu kufanyiwa.
 
Salaam wana Jamvi,
Katika hali ya kushangaza, picha hapo chini ni kitasa chamlango wangu nilionunua wiki 2 zilizopita. Kariakoo, risiti ninazo (TZS 100@230,000=2.3million). Cha kushangaza ni kwambazinasambaratikavyenyewe(bila kugongwa). Cha kushangaza niliporudikwa muuzaji badala ya kunionea huruma, ananiambia risiti imeandikwa maliikishauzwa hairudishwi, ilibidi niwe mpole kama mama lishe!!
Msaada: Naombeni msaada sehemu muafaka/dukana aina ya kitasa imara nay a kudumu kabisa, hata kama ni expensive siyoissue(quality speaks better than quantity).

mkuu kwa hesabu hizo utakua hujatepeliwa.au labda iwe ni makosa tu yakimahesabu.
 
Salaam wana Jamvi,
Katika hali ya kushangaza, picha hapo chini ni kitasa chamlango wangu nilionunua wiki 2 zilizopita. Kariakoo, risiti ninazo (TZS 100@230,000=2.3million). Cha kushangaza ni kwambazinasambaratikavyenyewe(bila kugongwa). Cha kushangaza niliporudikwa muuzaji badala ya kunionea huruma, ananiambia risiti imeandikwa maliikishauzwa hairudishwi, ilibidi niwe mpole kama mama lishe!!
Msaada: Naombeni msaada sehemu muafaka/dukana aina ya kitasa imara nay a kudumu kabisa, hata kama ni expensive siyoissue(quality speaks better than quantity).

Mkuu vilikuwa 10 au 100? Maana hesabu yangu imegoma kabisa! Labda kama vilikuwa vinauzwa 23,000/= Turekebishie kwanza hapo mkuu ndo tuendelee!!
 
Hivi inakuwaje mkishapigwa na mnakuja kuweka post?ilikuwa na kizuizi gani kabla ya kununua ungeweka post kuwa unatafuta vitasa?kuna wana jamvi humu wana maduka na wangekushauri aina bora ya vitasa na sio "bora vitasa" Pole lkn kwa ushauri nenda polisi kuna sharia inayoruhusu kurudisha mali dukani baada ya kununua hizo risiti zao na longo longo wala lisikutishe

Mkuu,umenistua kweli,hiv tunaongozwa kwa SHARIA au sheria au ulimi umeteleza mkuu,
 
Watz. hupoteza hela nyingi kwa kutapeliwa bila kujua lakufanya. Wakati mwingine ni kudharau mambo madogo madogo. Utakuta mahali pamendikwa usikojoe hapa, halafu unaona mtu anafanya kinyume chake.

Nilikuwa kwenye mkutano wa shule ya mtoto wangu. Tukaambiwa kuna wazazi wengi tu wametoa hela cash kwa mhasibu, na sasa kakimbia. Instruction ni kwamba shule haipokei cash. Sasa wanaambiwa hawajalipa ada wanashangaa . Hata risiti ikiandikwa vile ,haina maana uuziwe boya. Una haki ya kurudishiwa hela yako. Risiti ya TRA haiandikwi upuuzi kama huo. Nenda akupe risiti ya TRA.
 
Assa Abloy wako hapo mwenge kanunue kwao
 
Back
Top Bottom