Msaada: Nimetupiwa kipande nateseka mwaka wa 3 sasa, nahitaji msaada

Wewe Even MOre kuwa sawa ni simple sana.

Unachopaswa ni kufunguka zaidi kuhusu...
unapatikana mkoa gani?
Mazingira unayoishi yakoje?
Watu wako wa karibu ni akina nani?
Wewe ni dhehebu gani?

Ili usaidike mazima kwa nguvu ya MUNGU aliye juu zaidi.
 
Kwa namna ulivyoandika mtu hawezi kuelewa mkuu, ila kama ni mambo ya giza na hata mengine yoyote usihangaike kwa waganga, chukua muda piga magoti omba kwa Mungu atakusaidia hapo hauhitaji kupoteza hela yako maana ameahidi kutusaidia

ISA. :41:10
usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu

NB: Hayo matokeo siyo ya kumtendea mwenzako vibaya ikiwa ni hivyo Nenda upatane naye kwanza
 
kipande ndiyo nini?ila jaribu kufanya maombi hasa saa 6-8 usiku pia funga siku 7,mungu hamtupi mja wake nilikuwa kama wewe nilienda sana kwa waganga mwisho wanakwambia uwe kama wao kutokna na majini uliyo nayo mara nyingi hawakusaidii ila wanakupa unafuu wa kukuangamiza.

huna kipande,wala kitambulisho omba kwa imani yako...omba kupitia shida walizokuwa nazo mitume wao ndiyo kiigizo chetu mfano nabii Muhammad alirogwa ila mungu alimpa dua ya kusoma hivyo utasema kwa imani yako kuwa mungu mtume fulani alikuwa ni mwenye matatizo kadhaa wewe hukumuangusha ila ulimuinua kwa maadui na mimi naamini uwepo wako ndiyo umenipa hili jambo na wewe unaweza kuliondoa kupitia maombi haya na funga hizi..

waganga msiwape utajiri wa bure.
 
Nenda Nachingwea
 
Nmerekebisha
Story ilikuwa nusu sasa iko kamili kasome tena
 
Ndg sijui ni nani wala watu gani wanaohusika ktk hili cz nimeambiwa ni kwenye masuala ya ki biashara
 
You can't serve Devil forever.
 
Soma hapa na uelewe nakutakia Kila la kheri katika Maisha yako mapya
 
Sina ujuzi wa maana za kitabibu lakini kipande ni pepo au jini wa kutengenezwa ambaye anatumwa kwa mtu na kunuiwa namna ya madhara ambayo ataenda kusababisha
Fanya kazi kwa bidii.
Soma media production na mambo mengine yanayohusiana nayo ili uwe more creative.
Jifunze biashara ya media.
utaona mabadiliko.
 
Fanya kazi kwa bidii.
Soma media production na mambo mengine yanayohusiana nayo ili uwe more creative.
Jifunze biashara ya media.
utaona mabadiliko.
πŸ™†πŸ»β€β™‚οΈ asee! Jaribu urudie kusoma vzr story nimeirekebisha nadhan utanielewa tu. Kifupi mimi ni experienced media producer VIDEO, GRAPHICS and Printing kwa ujumla wake na nina ofisi kabisa na haya matatizo yamenipata baada ya kufungua ofisi.
 
Nyie mnaobeza waganga na kutukuza wachungaji mnamaanisha nini?
Binafsi niliamshwa kwa dawa ya mganga,

Ndio nikazinduka toka Gizani, shimoni, vifungoni.

Nilipoanza kuendelea kujiweka sawa zaidi,
Kupitia njia za waganga, ikashindikana.

Nikaanza kufatilia kanuni za kuishi Kiuokovu,

Now namshukuru Mungu.
 
Icho kipande Ulicho Tupiwa Ni Jini Maiti. Ushaidi Ni izo Ndoto Mbili Ulizo Taja Kuota Unazikwa Au uko Msibani, Tabia Ya Jini Maiti Nikuzika Kuanzia Mawazo Yako Unayo Waza Kichwani, Inaonekana Ilo Jini Limekaa Kwenye Mlango Wako Wa Aja Apa Na Maanisha Matamanio Yako Yale Unayo Taka Aya Timiii. Ila Kumbuka Mtu Wa Mbali Awezi Kuloga Chunguza Ukoo Wako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…