Msaada: Nina kucha ngumu kama mbao

upupu

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2008
Posts
614
Reaction score
198
Wakuu hebu nisaidieni,

Hii inasababishwa na nini? Je ni ugonjwa au kawaida? Mi nimekuwa nina kucha Ngumu vibaya mno, siwezi kuzikata na kiwembe zikikua, nail cutter ndogo huwa zinavunjika, labda zile kubwa ndo zinahimili.

Sasa je, hii inasababishwa na nini? Je ni Tatizo kiafya?
 
Kama ni za miguuni, vaa viatu vya kufunika muda mwingi.
 
Ningezipata hizo maana zangu ni laini hata hazikui zinakatika mnoo
 
loweka kwenye maji ya machungwa!
 
Utakuwa na madini mengi ya Calcium. Inaonekana unakula sana vitu vya baharini kama samaki n.k. Kabla ya kukata kucha zako, ziloweke kwenye maji au fua nguo mbili tatu kucha zitalainika then u can cut them...
 
Dozi ikoje, machungwa mangapi na maji kiasi gani ya kuchanganya, na naloweka kwa muda gani,

Chungwa moja kwa lita moja ya maji...loweka kwa nusu saa!

Alternatively ni limao ila acid content yake ni kubwa itabidi uongeze maji!
 
Jaribu kutumia kisu, mkasi wa bati au mkasi wa michongoma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…