Msaada: Nina safari ya Dar-Tanga, nataka kutumia RAV4 old Model

Msaada: Nina safari ya Dar-Tanga, nataka kutumia RAV4 old Model

lucky lefty

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2017
Posts
491
Reaction score
454
Wakuu habari zenu, nina kijisafari cha ghafla nataka kwenda Tanga kutokea Dar, naomba mnifahamishe vitu vifuatavyo Kwa wanaofahamu:

A) Mwendokasi wa Gari
B) Mafuta mpka Tanga Kwa Rav 4
C) Inahitaji kupumzisha gari kidogo au Naweza kunyoosha moja Kwa moja tu
 
A) Mwendokasi 100-120km/hr
B) 55ltrs yaani full tank utafika yakiwa yamebakia robo tank
C) Ukipenda japo siyo lazima unaweza nyoosha moja kwa moja

NB. Tochi, kwny 50 tembea 50

Asante Mkuu
 
Mkuu, nina jamaa yangu ana IST anaenda singida bila kupumzika sembuse tanga tena Rav4...we piga kiatu nonstop hadi tanga. Hapo ni masaa ma5 tu
 
Wakuu habari zenu, nina kijisafari cha ghafla nataka kwenda Tanga kutokea Dar, naomba mnifahamishe vitu vifuatavyo Kwa wanaofahamu:

A) Mwendokasi wa Gari
B) Mafuta mpka Tanga Kwa Rav 4
C) Inahitaji kupumzisha gari kidogo au Naweza kunyoosha moja Kwa moja tu
mkuu cha msingi angalia service hasa kwenye joint za mbele na pili zingatia vibao kwenye hamsini fuata hiyo barabara ina polisi balaa mkuu nimepita cku siyo nyingi , beba pia maji ya kutosha mkuu
 
mkuu cha msingi angalia service hasa kwenye joint za mbele na pili zingatia vibao kwenye hamsini fuata hiyo barabara ina polisi balaa mkuu nimepita cku siyo nyingi , beba pia maji ya kutosha mkuu

Pamoja Mkuu[emoji1545]
 
1. Mwendokasi utasaidia wewe kusave sana hela. HOW?
Kwanza fuata vibao vya barabarani. Kwenye 50KPH tembea speed hiyo hiyo ili usigombane na matrafick Wakachukua 30,000TSH zao. Na unaporuhusiwa above 50KPH tembea kati ya 80KPH to 120KPH. Usitoke kwenye hii range. Hapo ulaji wa mafuta utakua ni minimum. Vioo ukiwa umefunga. Vilevile angalia braking na acceleration zako. Usikanyage sana wese ili ukoleze gari mapema. Wese linaenda sana pale. Na epuka braking za ghafla. Unachakaza gari na hatari.
Kwahiyo speed ni muhimu kwa afya ya chombo, gharama na usalama wa wasafiri.

2. Mafuta lita 50 more than enough. Tukiassume una 2.0L car kwa hizo kilometer 350 za Dar to Tanga kwa hiyo gari ikiwa na consumption ya 10KM/L utatumia lita 35 tu. So utabakiwa na lita kibao tu za Misele. But kumbuka service ya gari, uendeshaji wa dereva (especially hapo kwenye acceleration ) kutachangia sana ulaji wa wese.

3. Huo umbali mfupi sana. Kanyaga moja kwa moja. Stop and go zinaongeza ulaji wa mafuta sana. Kwahiyo piga moja kwa moja.

Additional:
4. Ondoka mapema sana kama saa 10 asubuhi. Ukiondoka saa 12 utakua unafanya racing na mabasi ya mkoa. Sio viunbe wazuri wale.

5. Pitia njia ya Bagamoyo. Ni fupi zaidi. Kama huijui vizuri, tumia Google Map. BTW huwezi kupotea.

6. Kama mtakua wawili itakua poa zaidi. Njiani mambo mengi.

7. Usipige vichwa. Ile kuokota abiria wa njiani. Ondoka na mtu unaemjua kutokea DSM.

8. Usalama kwanza. Seat Belt, Usitumie simu huku unaendesha.

All the Best Bro.
 
nilishaondoka na gari kama hiyo hadi kahama, non stop, wewe unaongelea Tanga?
 
Tanga upumzishe gari? Hapo karibu sana. Jaza full tank na hakikisha tu gari iko fresh.
Kuwa makini kwa sababu magari ni mengi barabarani kwa sasa barabara hiyo mpaka Segera. Wale wenzetu wa kilimanjaro ndiyo wanarudi mjini so kuna wenye uzoefu na safari ndefu na wasio na uzoefu. Take care na nakutakia safari njema.
 
Gari kama MarkII Grande yenye cc2500 inaenda Dar na kurudi TA ikiwa full tank, so am assuming RAV 4 yenye ~2000cc ikiwa full tank itafanya the same...
 
Back
Top Bottom