Msaada: Njia za kuongeza au kunenepesha mwili

Al-shabaab

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2013
Posts
1,791
Reaction score
619
Habari zenu wana JF
Naomba msaada wa njia zipi mfano kama ni chakula au mazoezi yatakayosababisha mwili wangu kuongezeka
nitashukuru sana.
 
Aisee kuutafuta unene sio kazi,ishu ni kuupuunguza.
 
Zingatia msosi huu:
Asubuhi.
Chapati 3,supu ya utumbo,soda baridi moja ukishamaliza shushia na lita 1 ya maji bariiiiidiiiiii.

Mchana.
Chips Kuku,mayai mawili pembeni,soda baridiii,ukimaliza shushia maji baridi lita 1

Usiku.
Nyama nusu,ndizi 4 mshale,biereee 4 then ulale,fanya hvyo kwa mwezi utanenepa ukifikia unene unaoutaka unaacha.
 

hapo kwenye soda badili weka.bia
 
Habari zenu wana jf
naomba msaada wa njia zipi mfano kama ni chakula au mazoezi yatakayosababisha mwili wangu kuongezeka
nitashukuru sana.

Njia zinazo weza kukusaidia kuongeza unene
1.Kula chakula cha kutosha kila unapokula halafu chenye mafuta mengi,chakula chenye wanga zaidi nk.
2.Usikae muda mrefu bila kula chakula,muda kabla ya mlo mwingine usizidi masaa 4 au 3 halafu ukipata msosi kandamiza sawasawa.
3.Achana na mazoezi hasa yale ya kukimbia.
4.Kula chakula kingi kabla ya kwenda kulala.
5.Punguza mawazo
6.Punguza kula mboga za majani na matunda badala yake kandamiza nyama,maharage
Na Kutumia njia za kawaida ni bora kwa sababu ukiona uzito umezidi una achana na njia
hizi lakini unene wa dawa wakati mwingine hata kama ukiacha kutumia zinakuwa
zimeathiri mfumo wa asili wa utendaji kazi wa mwili huenda ukashindwa kuzuia tena.
7. Ukitaka kunenepa kula kwa wingi Ufuta mweupe mbichi changanya kidogo na sukari au pia waweza kupika huo ufuta ikawa ndio chakula chako utanenepa mwili wako.
 
Habari zenu wana jf
naomba msaada wa njia zipi mfano kama ni chakula au mazoezi yatakayosababisha mwili wangu kuongezeka
nitashukuru sana.
mwili una faidagani kwako wakati una afya? Au mwenzi wako anapenda wenye mwili mkubwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…