Msaada: PC (hp) imezima ghafla baada ya kuchomeka waya wa Sub-Woofer

Jay wa Jay

Member
Joined
Feb 4, 2013
Posts
71
Reaction score
64
Kama kichwa kinavyojieleza wadau. Nimechomeka waya wa Sub-Woofer ambayo ilikuwa imewaka (2 in 1) kwenye pc aina ya hp, ghafla ikazima... na haijawaka tena hadi hivi sasa.

Nimejaribu kutoa betri na kuiwasha ikiwa imechomekwa moja kwa moja kwenye chaja, taa ya chaja inawaka, lakini pc haiwaki hata kidogo.

Msaada tafadhali.
 
Sawa endelea kusikiliza mziki bila Kuunganisha Sabufa.
 
Hiyo itakuwa imejishort, mi yangu nilikua nachomoa waya wa buffer ikajishort system ya sauti hadi leo ni hp pia
 
Ishaugua hiyo mm ilikua hivo hivo Pole Sana
 
Sabufa za mchina zinaua sana simu...sikujua kama na pc ni hivyo hivyo
 
Jamani kuweni makini sana. Haya masabufa mengi hayana Earthing. Huwa yana Voltage leakage kwenye connection media zake. Sasa kama huo waya ukiishika unapigwa short unategemea ukiweka kwenye pc nini kitatokea??? Kuna shida sana kwenye music systems hasa hizi ambazo ziwnuzwa 120k [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] jaribu kuwa na music system yenye wireless connectivity eg. Bluetooth, NFC, DLNA au Optical kwa kuwa ni salama zaidi kuliko Wired cabling
 
Tatizo sio kubwa sana inabidi umuone fundi,power supply itakuwa ime cut power to prevent damage.
Zima laptop.
toa power cable.
toa battery.
bofya power button for 45 sec.
rudisha power cable.
rudisha battery
turn on your laptop.
 
Tatizo sio kubwa sana inabidi umuone fundi,power supply itakuwa ime cut power to prevent damage.
Zima laptop.
toa power cable.
toa battery.
bofya power button for 45 sec.
rudisha power cable.
rudisha battery
turn on your laptop.
Mkuu fafanua vizuri hapo, maana ya kwangu pia imezima ghafla nilipokuwa nachomeka power cable, ina week sasa haitaki kuwaka.
 
Hiyo itakuwa imejishort, mi yangu nilikua nachomoa waya wa buffer ikajishort system ya sauti hadi leo ni hp pia
Mi yangu pia, dogo kavizia sipo kabeba PC kaunga na Woofer ale mziki. Ikakata sauti mazima mpaka leo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…