Msaada please: Mimba hii isipotoka italeta madhara kwa mwanangu, nifanyeje?

Bonlove

Member
Joined
Feb 2, 2012
Posts
45
Reaction score
5
Wanajamvi naombeni msaada mke wangu ananyonyesha (ana mtoto mdogo) katika cheza cheza yetu alikosea kuhesabu siku zake leo ni siku ya 5, bilabila hajaona siku zake ikabidi niingie dukani kununua urine test baada ya kupima ana ujauzito sasa na yule mtoto..

Itakuwa balaaa naombeni ushauri ila plan yetu ni kutoa hiyo mimba bt njia ya kutoa hatufahamu msaada plse
 
huyo mtoto ana miezi mingapi?mke wako akatishe kunyonyesha ili atunze ujauzito moja,la pili mwanamke aliyeishazaa si vizuri kutumia mzunguko wa hedhi kama njia ya uzazi wa mpango mara nyingi inadunda.
 
Nijuavyo mie kunyonyesha kikamilifu penyewe pia ni njia moja wapo ya uzazi wa mpango,au mkeo hamnyonyeshi dogo ipasavyo?
 

Usithubutu kutoa mimba lea watoto watakuwa we si wa kwanza kukosea
 

We unaogopa macho na maneno ya wanadamu yeye aliyekupa uhai humwogopi,kwa nini ukatishe maisha ya kiumbe kisicho na hatia kwa kuogopa watu na upatapo tatizo hao hao wa kwanza kukucheka.
 
We unaogopa macho na maneno ya wanadamu yeye aliyekupa uhai humwogopi,kwa nini ukatishe maisha ya kiumbe kisicho na hatia kwa kuogopa watu na upatapo tatizo hao hao wa kwanza kukucheka.

Pokea "likes"
Umeandika maneno ya busara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…