Msaada: Ratiba za minada ya wiki mkoani Dar es Salaam

Hiyo mnayoiita minada sio minada ni MAGULIO. Gulio ni sehemu panapuzwa bidhaa mbalimbali siku maalumu ya wiki. Minada ni sehemu wanyama wanapouzwa. Kwa dsm. Minada ni Pugu. Vigwaza, Pwani pia ni mnada. Mnadani ukinunua mfugo unatozwa ushuru. Vingungutinsio mnada kwa sababu pale wanapouza mbuzi wanauza kinyume cha sheria. Na mbuzi wale wanakuwa wamenunuliwa Pugu mnadani.
 
Ahsante kwa ufafanuzi makini
 
Kibamba mbuzi choma Ni jumatano na jumapili.
Loliondo mbuzi choma Ni jumamosi.
Vigwaza mbuzi choma ORIGINAL +++ Ni alhamisi.
Fuatana namimi. Angalizo, kwenye mbuzi choma kote Kuna beer.
Kibamba hakuna gesti.
Mkuu hao mbuzi choma wanakuwa mnadani au wanakuwa kwenye bar?
 
Huu mnada unawatu wengi sana kila alhamus napata shida sana kupita pale jioni ninaporudi kutoka job.
Sana siku ya alhamisi ni fujo ila ndio utafutaji maisha lazima yaendelee. Vitu bei chee
 
Sijui Unakaa Wapi?Utachagua Mwenyewe Mnad wa Kwenda

Jumatatu Kinyerezi na Bagamoyo

Jumanne Ni Tabata Balakuda Boko na Kivule

Jumatano Chanika Kibamba CCM na Kimanga

Alhamisi Kigamboni Bunju na Ukonga Moshi Bar

Ijumaa Kitunda Majohe ya Viwege na Bunyokwa

Jumamosi Pugu Kinondoni Biafra na Loliondo Kibaha

Jumapili Geza Kigamboni na Sala sala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…