Nauli ya basi Makambako mpaka Songea ni elf 20 (5hrs) songea to Tunduru hakuna basi kubwa bali kuna landrovers nauli elfu 22(rough road).
Mwisho kwa tahadhari zaidi zingatia ulinzi na umakini mara uwapo songea, ukiwa bar, hotel, njiani acha kujionyesha kama ni mgeni sana au una pesa nying kwani huu mji kwa mauaji ndo usiseme.
Umeona yanayojiri leo.
Njia ni mbaya sana...kipindi cha mvua ni worst!Nashukuru Mkuu Kayako; kwa hiyo njia ya Songea - Tunduru magari makubwa hayawezi kupita?, kwa nini hakuna mabasi makubwa yanayopita njia hiyo - abiria ni wachache au njia ni mbaya sana?.
Hivi White house siku hizi siyo famous tena...? halafu huko msamala ni nje sana ya mji!kwa Songea karibu sana mkuu. Ukifika unaweza kulala Top one pale msamala chumba elfu 30 (chukua tahadhali na vitasa vya mlango huwa mara nyingi vimetobolewa katundu for chaboringing). Toka songea mpaka tunduru ni barabara ya vungu na it take 8-10hrs hasa hii masika.
Kwa vivutio songea waweza kwenda ukumbi wa mashujaa ambapo wale majimaji heroes taarifa zao zipo pale.
Njia ni mbaya sana...kipindi cha mvua ni worst!
Kwa magari ya abiria wengi wanaogopa kupeleka mabasi yao huko kwa sababu ya barabara. Walau Landrover "zina roho ngumu" ndo mana zinaweza kwenda huko.Asante Mkuu Mkeshaji; nafikiri kipindi cha mvua huko ni Nov - May. Vipi katika miezi mingine unaweza kupita na gari kubwa kwa shida au haipitiki kabisa. Kama haipitiki kabisa vipi mazao wanasafirisha vipi au huko hakuna bidhaa yeyote inayozalishwa?? Sitaki kujipatia majibu mepesi kwa swali gumu kama hili, samahani mkuu...!!!
Usisahau kubeba camera ututumie masinepu ukirudi.........tuijuwe nchi yetu vizuri
Kibiti zipo guest house lakini si nzuri sana.Nakushukuru Mkeshaji; kwa taarifa za ziada kutokea Dodoma mpaka Songea. Hizi taarifa zinanisaidia kupanga safari yangu vizuri zaidi; asante kwa kunieleza kwamba kibiti ni mji mdogo na ninaweza kukosa guest house. Nakubalina na wewe na sasa nitapanga kulala Ikwiriri, haya maeneo nilishawahi kupita lakini zamani kidogo. Nakumbuka tulikuwa tunatokea Mtwara na landrover 109, ilitusumbua sana tokea Lindi mpaka Nangurukuru, huwezi amini hapo tulitembea usiku kucha na Nangurukuru mpaka kivukoni (kabla ya daraja) tulitumia mchana wote; hivyo basi tuliamua kulala ikwiriri, lakini kulikuwa giza hivyo sikupata hata kujua uzuri na ubaya wa mji huo, kwani tuliondoka alfajiri sana.
Kutoka Bagamoyo tutapita ile njia inayotokea Msata. Tarangire tunataka kwenda mbuga za wanyama, sijajua connection ya Tarangire - Ngorongoro iko vipi, naamini wakiingia watu wa Arusha wanaweza kunipa taarifa nzuri zaidi, ili ikiwezekena nipitie na Ngorongoro.
Tunajifunza mengi humu JF. Hii itatusaidia na sisi wengine tutakapopita maeneo hayo.
Mgombezi,
Kama utajaliwa kusafiri na kufika Songea, nifanyie yafuatayo njiani unapokwenda Tunduru;Uliza mito yote ya maji isiyokauka na ukipata majina yake itakuwa poa. Kisha nitumie.