Msaada tafadhali juu ya ratiba yangu

Kidasa

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2013
Posts
309
Reaction score
108
Wakuu wa JF,nina tatizo ambalo limekuwa linanisumbua,ipo hivi:

1.Nikikosa usingizi usiku kwa kiwango kisichotosha,ujue kesho yake nitashindwa kufanya kazi kabisa,unless ninywe maji mengi sana,hata hivyo mwili wangu utakuwa katika khali ya ajabu sana.

2.Mimi nasoma,naweza nikalala vizuri tu,nikaamka saa 4.30 asubuhi kusoma kiukweli siwezi kuunganisha,inabidi atleast saa 12 asubuhi nirudi tena kulala.Nisipofanya hivyo mwili utakuwa katika khali mbaya sana.

3.Kwa khali hii imenifanya nifirie nitakuwa na ugonjwa wa BARIDI YABISI-RHEUMATISM.
 
Sikuelwa ishu yako sawasawa lakini sioni uhusiano wa moja kwa moja baina yaadalili ulizoweka hapo na rheumatism; inawezekan kiswahili yangu mbofumbofu nashidwa kujua ulichoandika.
 

Sijaelewa uhusiano wa kutolala na 'ugonjwa' unaoufikiria unao, Rheumatism! Labda ni kwa sababu mtu fulani katika familia/ukoo anao na wakati anao alikuwa na shida ya usingizi.

Kwa maelezo yako inawezekana hali yako ni kutokana na mfumo wa maisha(Mwanafunzi), na hivyo kuwa na ratiba fulani ya kusoma ambayo mwisho wa siku mwili wako huzoea na kuwa unakosa usingizi huo..pili mwili hufanya njia ya adjustment/regulation wakati wa Stress/Msongo na hii oia huweza kusababisha kutopata usingizi vyema, na kutofanya kazi vizuri siku inayofuata.

Lakini kwa hali hii, Sijaona dalili ya kusema unashida ya Rheumatism...Wakati fulani kukosa usingizi ni tatizo kiafya, yaani INSOMNIA, na hii pia inaweza kuwa Early Insomnia, Late Insomnia n.k Nikimaanisha wapo watu ambao wana maisha ya kawaida ambayo hayawahitaji kuwaamsha kwa ulazima wakati wa usiku na usingizi kupotea, lakini ifikapo muda wa alfajiri(hasa saa kumi) hukosa usingizi "usingizi kupaa" kabisa na kufanya wakae macho.

Hata hivyo, sidhani kama hili ni tatizo hapa kwa sababu ya mtindo/mfumo wa maisha unaokulazimu wakati fulani kuamka muda huo.

Adjustment ya ratiba yako, ni muhimu katika shida uliyoisema, na endapo hali itazidi nakushauri ufike hospitali.
 

Asante mkuu kwa ushauri wako,kwa nini nasema ni ugonjwa wa baridi yabisi kwenye mifupa,ni kwamba usingizi ukishanipaa ili kuufosi na mwili wangu kuurejesha ktk hali ya kwaida inanibidi nijifunike gubigubi na blanketi,inanibidi nivae hata na sweta au koti, kwenye mivupa yangu nahisi kunakuwa na ukakasi mpaka niueushe kwa joto ndio mwili wangu utakuwa vizuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…