Msaada tafadhali: Nahitaji kufanya huduma ya Uwakala wa Tigopesa na Mpesa

GARETHBALE

Member
Joined
Dec 22, 2013
Posts
76
Reaction score
333
Natumaini wote hamjambo, mimi pia sijambo, Tumshukuru Mungu.

Wadau nafikiria kufanya biashara ya Tigopesa na M-pesa, nataka kujua mtaji wa biashara hii, changamoto na faida ya biashara hii, eneo ni stand ya mabasi, naomba ushauri wadau.

Mungu awabariki wote.

Asante.
 

Biashara ni nzuri hasa kwa eneo ulilochagua.Faida ya hii biashara inaendana na kiwango cha kazi utakayokuwa unafanya,kadiri miamala inavyokuwa mingi ndivyo na faida itakavyokuwa kubwa.
Mtaji angalau usipungue 1 M kwa kuanzia ambapo unaweza weka pesa ya mtandaoni (float) laki nne kwa kila line yani tigo na voda na laki mbili ukabaki nayo pesa taslimu.

Changamoto kidogo imekuwa kwenye M-pesa hasa unapokwenda kujaza pesa kwenye simu yako kupitia Bank wanatoza charges kwa huduma hiyo ambayo kipindi cha nyuma ilikuwa ni huduma ya bure.

Changamoto nyingine ni utapeli hasa kama hautatunza namba zako vizuri unazofanyia kazi.Mfano watu wakiifahamu namba wanaweza kukuingizia ujumbe kana kwamba mtu ametoa pesa kumbe kiuhalisia haipo hivyo.Pia swala la kuchomekewa pesa bandia n.k

Karibu katika biashara ya kutoa huduma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…