Habari wakuu, Tatizo ni kwamba, mwanamke ana mimba ya miezi 4 ila ameanza kujisikia kukandamizwa kibofu cha mkojo, na anaweza kujisikia kama amebanwa na mkojo lakini akienda kukojoa anakojoa mkojo kidogo. Clinic wamemshauri akiona hali inaendelea, afanye vipimo vya Utra sound. Ningeomba kujua vipimo hivi vinapatikana Hospital gani kwa Dar es salaam, na kwa gharama gani. Nakaribisha michango yenu.