Msaada tafadhari

Msaada tafadhari

sometimes ni RSI( repetitive Stress Injuries) au spongelosis kwa kairuki wababaishaji sana hapo pole sana
 
ndugu yangu Tyta...unahitaji sana kuonana na Neurologist akahakikisha sio tatizo za mfumo wa fahamu. Yes inaweza kuwa tatizo la mifupa na/au viungo (Osteoarthritis) lakini kwa maelezo yako mafupi napata picha ya Neurology zaidi. Kairuki sidhani kama kuna Neurologist (wapo wachache sana hawa), nadhani ulionana na Orthopedician na ndio maana hata uchunguzi na utatuzi wake kukaa kimifupa/viuongo zaidi.

Tafadhali muone Dr Aris, anapatikana Muhimbili, lakini pia ana private clinic sijui wapi, ukimpata Muhimbili kama utataka kumuona huko kwenye clinic yake atakuelekeza. Ni Neurologist mzuri sana huyu na daktari mzuri sana pia. Nadhani kuna umuhimu wa kumuona haraka ili kama ni progressive neurologic disease uiwahi kama hujapata ulemavu. Pia nadhani unahitaji kuanza physiotherapy haraka ili kuregain strength katika mkono uliopoteza. Daktari atakushauri zaidi kwa hili.

Alternatively, unaweza pia kumuona Prof Matuja, naye yupo Muhimbili na ana clinic yake Upanga. Lakini first option ni kumuona Dr Aris. Goodluck.
 
Thanx wandugu,i wil try to see the neurologist
 
Fuata ishauri wa mkuu Riwa haraka iwezekanavyo...Mungu akubariki upone mkuu
 
Pole sana, kama walivo sema wengine kaonane na daktari akupe ushauri na tiba...
 
Wanajf,mimi ni kijana wa miaka 23,nasoma chuo mwk wa pili...nimekua nasumbuliwa na tatizo fulani kwa muda mrefu sasa(yapata miaka 3)..ni kwamba nimepoteza uwezo wangu wa kuutumia vyema mkono wangu wa kulia katika kuandika..mwanzoni haukua sirias sn,nilianza kutambua mabadiliko katika mkono wangu kupitia mwandiko wangu ambao ulianza kubadilika na kuwa kazi kusomeka..baadae nilianza kutumia excesive force na kugrip pen kwa nguvu alimradi nipate enaf presha niweze kuandika vizuri..siku zilivyoenda ndipo hali ilizidi kua mbaya kwani kuna wakati nilishindwa hata kukontrol movement za vidole vyangu wakati wa kuandika..maumivu husikia sehemu za joint kwenye vidole,shoulder joints na hata kwenye uti wa mgongo sehem ya chini kdogo ya shingo.maumivu si wakati wote.uwezo wa kuandika kawaida umepotea kabisa kwa sasa.i hold the pen so weird during writing nowdays.nimeenda kwenye vituo vya kama dr.kairuki,ocen road,na kupimwa damu kuangalia kama nina upunguvu wa madini,tatizo la figo na hata xray..walichonifahamisha kwnye xray ni kua nina tatizo la shoulder osteoarthritis,nimepewa dawa lakini sijapata nafuu.before nilishawi kutumia dawa kama neurotin na nyingine za nerves.nimejaribu kuelezea kwa urefu japo inaweza kuwa ngumu kueleweka kwa tatizo hili sijawahi kumshuhudia nalo mtu mwingine..kuna wakati nilihisi nina tatizo linaloitwa writer's cramp,bt kwa dalili zake nyingi sina.tatizo hili ni wakati wa kuandika tu.natanguliza shukrani kwenu na ningependa nipate kujua walau mwenye tatizo kama hili au aliyepata mshuhudia mtu mwngne alikabilianaje nalo.

Habari ndugu, vipi ulifanikiwa tupe mrejesho kwani wenye matatizo tupo wengi!
 
Miaka 23, mwaka wa 2011
kwa hiyo sasa hivi utakuwa una miaka 27, big up! mkuu vpi? lakin ulitatua tatizo lako mkuu Tyta.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom