Msaada: Tarehe ya kujifungua imepita lakini dalili bado, tatizo nini?

Kirumi

Member
Joined
Sep 23, 2012
Posts
6
Reaction score
2
Ndugu zanguni, wanabodi!

Mke wangu ni mja mzito na kwa mujibu wa clinic yake na amepima pia kile kipimo cha utra sound na ikajulikana kwamba angejifungua tarehe 3 ya mwezi wa nne, cha ajabu hadi leo tarehe 10/4 bado hajajifungua na wala bado zile dalili hazipo.

Naombeni msaada na ushauri kuhusiana na hili tatizo, je tatizo la kiafya au ni kawaida?
Hii inanifanya mimi na yeye pia tuishi kwa wasiwasi mwingi hasa ukizingatia kwamba hii mimba yake ya kwanza.

Thanks and best regards!

Kirumi.
 
Zikipita siku 14 mpeleke hospitali au unaweza kumpeleka hata sasa anawekewa dripu ya uchungu + kutobolewa chupa ya mtoto ili ajifungue
Vitu unavyoweza kufanya kusaidia kuongeza stimulation ya oxytocin
  1. Changanya

  • maji 1,5liters
  • maji ya malimau 2,
  • vijiko2-4 vya supu vya asali,
  • vijiko viwili vya supu tangawizi,
  • vijiko 2 vya chai vya cayannepepper.
Anywe nusu,asipohisi kitu amalize kilichobakia
2.Tendo la ndoa linasaidia kuongeza stimulation ya homoni ya oxytocin,shahawa zina prostaglandin nyingi ambazo hufanya kizazi kilainike
3.Atembee au apande na kushuka ngazi w,uzito wa kichwa cha mtoto unapogusa shingo ya kizazi inaongeza stimulation ya homoniya oxytocin
 
Dont Worry!
Sio kila mtoto anazaliwa kwenye due date iliyoainishwa.....some wanajifungua within two weeks kabla...au baada...ingawa mimi nilibahatika kujifungua tarehe ile ile.....atembee sana...itamsaidia...ALL THE BEST!
 
Kaka hongera sana. Lakini usiogope kwa mama ambae ni ujauzito wa kwanza huwa kunaweza tokea kupitisha siku na ndio maana ile tarehe ya kujifungua huwa tunasema ni expected date kwamba ni tarehe ya matarajio. Lakini cha msingi fanya maandalizi muhimu pia afanye mazoezi ya kutosha hiyo itamsaidia sana na mtakapoona kuna mabadiliko yoyote yale muwahishe hospitali. Mungu awatangulie na shemeji ajifungue salama.
 
Mama anatakiwa kufanya yafuatayo! Mazoezi kwa sana, tendo la ndoa angalau mara kadhaa, hii yote ni kuongeza njia ya kizazi kwa ajili ya mtoto kupita! Kama inawezekana awe hospitalini kwa ajili ya uangalizi zaidi ikiwa na kuwekewa kiongeza uchungu au Oxytocin! Mama akizingatia haya ataepuka kupelekwa Caessarean kwa operation! Kila la kheri
 
kama unaamini kuna Mungu. Mlete kwa Mama mwakatare atafunguliwa kwa jina la Yesu. Nimeona na nimeshuhudia wengi wakifunguliwa baada ya kuombewa. Nawakilisha
 
kama unaamini kuna Mungu. Mlete kwa Mama mwakatare atafunguliwa kwa jina la Yesu. Nimeona na nimeshuhudia wengi wakifunguliwa baada ya kuombewa. Nawakilisha

mmh,mkawainue wanaoshndwa kuinuka mnh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…