Msaada tatizo la kutokuona kila ifikapo jioni

Msaada tatizo la kutokuona kila ifikapo jioni

Chuji W W

Member
Joined
Mar 29, 2017
Posts
39
Reaction score
37
Wadau kwanza poleni na majukumu yote ya kupigania maisha, naombeni kufunguliwa macho juu ya tatizo tajwa kunakijana (mtoto wa sister ni darasa la 7 sasahivi) nimemkuta na hii dhahama na kwa mujibu wake ni tatizo la kudumu (toka utotoni) yaani ikifika jioni ya saa 12 haoni kabsaa ila asubuhi na mchana safi kinachoniuma zaidi darasani ni kichwa tegemezi baba na mamayake ni marehemu hvyo kwa anaejua plz msaada wa mawazo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Atakuwa ana ukungu kwenye macho...

Nyakati za mchana anaona kwa sababu kuna mwanga wa kutosha, jioni kwenye mwanga hafifu macho hupoteza uwezo wa kuona kwa sababu ya either utandu au ukungu kwenye macho...

Aende hospitali wakamchune macho... Au kuvalishwa lens...


Cc: mahondaw
 
Nafikiri Hilo tatizo lilishawahi kunitokea Back in 2011 yaani usiku Huoni kabisa unaeza Paramia adi Mti ila sasa cha kufanya embu asile maharage na mwandalie Mboga za Majani za Kutosha na anywe maji ya Kutosha!
 
Niliwahi kupata tatzo hilo mwaka 2004. Nikiwa boarding school. Nilienda hospital walinipa miwani hata hivyo nilivaa kidogo tu, tatzo likaisha nikatupa miwani kulee
 
Mpe karoti kwa wingi
juisi ya spinach japo kwa wiki mara 2
Ale mchanganyiko wa matunda kila aiku kwa siku 7
Anywe maji glass moja mara tu akiamka kabla haja swaki kinywa.
FANYA HIVYO KISHA LETA MREJESHO
 
Umeshampeleka hospitali? Mimi naona hyo ndo ingekua ishu ya kwanza.
 
Back
Top Bottom