Msaada Toyota Voltz au Honda CR-V

Futa kwenye mawazo yako hiyo Honda CR-V. Ni pasua kichwa
 
Tofauti na spare parts hakuna shida nyingne ya hio Honda consumption ya mafuta ipo vzur kma una connection ya mtu wa parts toka Japan ucwaze nunua
 
Chukua Toyota Volts utafurahi
Wakati anaiagiza mwambie mapema atafute access za wauza vipuri vya hayo magari hasa body parts,akitaka kujua ubaya wa hilo dude bahati mbaya avunje headlight moja na bumper la mbele aisikie bei yake..kama mtu huhitaji gari ya show off chukua Rav4 1999/2000model ni gari nzuri.
 
Sioni issue hapa ya kujinasibu sana. Hatujali origin yake n.k tunajal ipo chini ya TOYOTA na spares zake zinapatikana na inaitwa TOYOTA VOLTZ. So si kuwa tu ukisoma google kitu iwe issue kubwa sana.kuwa na asili au kutengenezwa marekani hakuiondoi sifa yake ya kuwa ni Product ya TOYOTA TECHNICALLY. Hizo porojo nyingne hazibadili chochote hata kidogo. Maana kuna siku tutabishana kuwa na harrier au prado si ya japan sababu moja ya mafundi wake wana asili ya uingereza so si ya mjapan


 

Nimekuelewa vyema mkuu.

Asante, na ninaomba kwa kila niliyem mislead kwa bandiko langu anisamehe bure, Voltz ni Toyota.
 
Imeandikwa touota, na la msingi ni inakidhi vigezo vya mleta mada, mafuta, ubora na upatikanaji wa vipuri.
Acha kukariri mambo ya GM Motors!

Mkuu kuna post nimeweka hapo juu ya kuwataka radhi baada ya kuelewa, asanteni kwa kunielewesha.
 
Nimekuelewa vyema mkuu.

Asante, na ninaomba kwa kila niliyem mislead kwa bandiko langu anisamehe bure, Voltz ni Toyota.

Binafsi naipenda na niliifuatilia sana mtandaoni nikapata kitu. Wamarekani wamemtumia mjapani kuuza hayo magari na wakatia nembo ya toyata then ikawa Toyota Voltz.
Kwa ulaji wa mafuta zipo Voltz za aina 3 ambazo ya kwanza inatumia mpaka km 11 kwa 1ltr na nyingine mpaka 12km/ltr na 13km/ltr kutokana na ukubwa wa Engine. Ki ujumla imekaa vizuri sana but wasiwasi ni vipuri tu hasa bumper la mbele ambalo huwa naona linachoka mapema.
 

Safi sana mkuu, naona watu wameishia kushambulia badala ya kujieleimisha.

Ukisoma vizuri michango ya watu humu kuna jamaa ametahadhalisha sana kuhusiana na bodi kwamba spare zinaweza kusumbua.

Otherwise itakuwa ni gari nzuri, probably.
 
Haiwezekani hizo gari aina tatu tofaut yake iwe eti ni lita moja moja hiyo ni tofaut ndogo sana ambayo si lazima iendane na engine. Fatilia vizuri na tafuta tofaut za ukwel acha hizi za layman.

 
mkuu kama voltz sio toyota ni nani sasa??

acha kukalili maisha mkuu rav 4 old model leo bado unaziwazia?? huko wazungu washakimbia zamani sana mzee
Kumbe na wewe ni mzungu?
 
Ila hii gari (Toyota Voltz) ina umbo tamu aiiisee.
 
Achana na kitu inaitwa Toyota Voltz iko poa sana
 
Aisee nilikua nimekubaliana kununua Toyota Volts Mil15 Yard sasa nabadili mawazo ngoja nitafute ki RAV 4
 
Sijui nna matatizo sijawahi kuipenda Toyota voltz
 
Huna matatizo mkuu ni roho tu haijapenda,mbona kuna watu hawaipendi Prado.
 
Haka kagari (Toyota voltz) ni katamu, kana show nzuri mafuta ni wastani wa km 11 au 12 kwa lita, spear zinapatikana, cc1790, hii ninayotumia ni 4wd , kuhusu body parts sijaua kwa sababu sijaharibu bado lakini inawezekana ni ngumu kupatikana sababu hazijawa nyingi sana mtaani.
 

Mkuu kwa sasa usipate shida beforward wanaimport kila aina ya spare part within 30 unapata kifaa chako fresh kabisa.
Ninachoipendea voltz ina nafasi kubwa sana ndani,nyingi zina 4WD,Iinakula mafuta vizuri,iko stable road tofauti la RAV 4,ipo juu,ile dash bodi upande wa dereva ni kama harrier new model.
 
hello, boss unatumia ya mwaka gani, na uliipata kwa bei gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…