Msaada tutani, nina gari yangu aina ya Noah sr40 je nije/niende mkoa gani nikafanyie kazi ya kubeba angalau abiria?

karume msaka

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2018
Posts
412
Reaction score
721
Habari ndugu zangu!

Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu. Nipo hapa mbele yenu kuomba ushauri kutokana na Hali iliyopo ya kimaisha kwa sasa nimeona niitumie gari yangu aina ya NOAH Ili kujiingizia kipato.
Lakini sifahamu nianzie wapi na niishie wapi hivyo naomba ndugu zangu kutokana na umbali/utofauti wa mikoa tunapotoka naombeni mnipe madili ili nije nipambane familia isilale njaa

Gari ina Hali nzuri na inafika mkoa wowote hapa tanzania.!
Kwa mwenye kunipa dili anaweza liweka hapa hadharani ama hata kunifuata inbox kwa maelekezo zaidi

Natanguliza shukrani.
 
Jiandae kupakiza abiria waliobeba kuku, mbuzi na bata, baada ya mwaka ni mkweche. Mikoani hawatumii noah mpya mpya, bali kuukuu na nyingi ni manual sio automatic.

Kila la kheri Tanzania kubwa, watakuja wazururaji humu wakupe muongozo zaidi.
 
Gari yako Bado ipo yard mbona haina plate number!??
 
Nzega au Kahama
 
Jiandae kupakiza abiria waliobeba kuku,mbuzi na bata,baada ya mwaka ni mkweche ,
Mikoani hawatumii noah mpya mpya ,bali kuukuu na nyingi ni manual sio automatic.
Kila la kheri Tanzania kubwa watakuja wazururaji humu wa kupe muongozo zaidi
Kuna mkoa niliendaga nikakuta noah ni Automatic, je gari itawahi kufa ama!
 
Kila la kheri kwani mimi ndie nimekuambia naanza ruti?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…