rubii
JF-Expert Member
- Feb 22, 2015
- 14,032
- 18,540
Habari zenu wakuu
Nimekua na mambo yananisumbua zaidi ya mwaka sasa, na nimeweza kuwa mnafki na kuyaweka moyoni tu bila kuongea kwa watu mambo hayo.<br>
Kutokana na mambo mengimengi nilijikuta siwezi kulala usiku bila kumeza dawa(piriton)
Mwanzoni nilichukulia kawaida lakini sasa naona hali inazidi kuwa mbaya zaidi nilianza na vidonge viwili sasa nimefikia vitano.<br>
Kila siku usiku ni lazima nimeze vidonge hivyo kama nahitaji kulala na vimekua msaada mkubwa kwangu
Lakini sasa vinanitesa, Mapigo ya moyo yanaenda mbio mda wote natoka jasho kama glass iliyotolewa kwenye jokofu, Nahisi kizunguzungu mara kwa mara na giza la gafla hata imefikia kuanguka anguka. <br>
Ndugu wamekua wakiulizana nini tatizo nashindwa kuwaelezea tabia yangu ya kubwia mavidonge kila usiku, na nisingependa watu wafahamu napitia nini katika nafsi yangu. <br>
Nifanyeje niweze kuacha matumizi ya dawa hizi??
Je nikiendelea na ulevi huu nini mwisho wangu??
Nimekua na mambo yananisumbua zaidi ya mwaka sasa, na nimeweza kuwa mnafki na kuyaweka moyoni tu bila kuongea kwa watu mambo hayo.<br>
Kutokana na mambo mengimengi nilijikuta siwezi kulala usiku bila kumeza dawa(piriton)
Mwanzoni nilichukulia kawaida lakini sasa naona hali inazidi kuwa mbaya zaidi nilianza na vidonge viwili sasa nimefikia vitano.<br>
Kila siku usiku ni lazima nimeze vidonge hivyo kama nahitaji kulala na vimekua msaada mkubwa kwangu
Lakini sasa vinanitesa, Mapigo ya moyo yanaenda mbio mda wote natoka jasho kama glass iliyotolewa kwenye jokofu, Nahisi kizunguzungu mara kwa mara na giza la gafla hata imefikia kuanguka anguka. <br>
Ndugu wamekua wakiulizana nini tatizo nashindwa kuwaelezea tabia yangu ya kubwia mavidonge kila usiku, na nisingependa watu wafahamu napitia nini katika nafsi yangu. <br>
Nifanyeje niweze kuacha matumizi ya dawa hizi??
Je nikiendelea na ulevi huu nini mwisho wangu??