Msaada: Vifaranga wanaishiwa nguvu miguuni

vakolavene

Member
Joined
Jan 20, 2017
Posts
39
Reaction score
26
Habarini wanaforum.

Naombeni msaada nimefuga vifaranga wa kuku wa kienyeji 75 yapata wiki ya pili sasa.Ninawatunza kisasa ndani ya chumba maalumu nikiwapa huduma zote za kuku wa kisasa.

Sasa wiki iliyopita niliona baadhi yao wameanza shusha vibawa vyao. Nikaenda duka la madawa ya kilimo na mifugo, nikaelezwa na muuzaji niwanunulie Esb3 30% yawezekana wana magonjwa ya tumbo. Nilifanya hivyo nikawapa kwa siku tatu kwa kadri nilivyoelezwa, baada ya kumaliza nikaenda kumpa taarifa kua nahisi wanaendelea vizuri, akanishauri pia niwape multivitamin kwa siku tano, nikafanya hivyo na leo naandika thread hii ndio siku ya tano.

Lakini kuna utofauti nimeanza kuuona juzi baada ya kifaranga kimoja kuishiwa nguvu za miguu., ikabidi nikitenge, leo tena alfjiri wakati nawabadilishia moto takribani vifaranga 5 navyo havina nguvu kabisa, nimevurugwa nahisi kama nitawakosa wote. Naombeni msaada nifanye Nn na tatizo litakua Nn?
Tafadhali wanaforum.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Reactions: MC7
Mkuu hapo kwako kama unaeneo kwa nje ambalo chini halijasakafiwa,fanya kutafuta ule waya wa fensi ya kuku na utengeneze kama kiboksi kulingana na idadi ya vifaranga vyako na hapo unakuwa unaviweka vishinde baada ya jua kutoka na jua linavyozama ndio unaviingiza ndani ili vipate mwanga na vitamini ya jua pia kuna madini watayapata kwenye udongo hapo utaona wanavyoenda vizuri hadi utashangaa.

NB:mimi ni mfugaji na natumia njia hiyo kutunza vifaranga wangu huwa siwapi dawa yoyote zaidi ya maji,chakula na mboga za majani ni mwendo mdundo hadi vinakuwa vikubwa mwishoni mwa wiki navikologea shubiri mwitu kwenye maji vinakunywa.

-Ndumilakuwili-
 
Kwanza hakikisha wanapiga vitamini, pili lazima wapate chakula chenye madini ya chuma na calcium mfano dagaa na chokaa..!

Chunguza waweza wakawa wanaumwa pia hasa mafua au gumboro km haujawapa chanjo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Choo inaziba vinashindwa kujisaidia?
 
Wawekee pia calcium inaweza ikawa ndio sababu. Kuna ile yakuchanganya kwenye maji kabsa innafanya kaz haraka zaidi.
 
Asante kwa ushauri ndugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…