Msaada wa Daktari Bingwa

v4c

Member
Joined
Oct 19, 2012
Posts
17
Reaction score
3
Wakuu tuna baba yetu anatatizo la kuvimba miguu na tumbo kujaa na moyo unamatatizo pia hali kabisa chakula, sasa tumepima hospital wamesema figo zinamatatizo pia tumboni kumejaa maji so inabidi tukanyonye hayo hospital, sasa kama kuna mtu anamfahamu dokta ambaye ni bingwa kwa mambo hayo na hospital anayopatikana naomba tusaidiane jamani
 
Poleni sana mkuu.......hapa JF utapata msaada wa kutosha....vuta subira......
 
pole sana mconsult dr.mbembati wa nh2

mbembati?! Labda ni tofauti na ninayemfahamu miye. Nendeni mnh mtahudumiwa. Mtapeleka hospital zingine wakamfanyia tapping aafu akafa. Hatuna hakika kama tatizo alilo nalo ni figo, moyo au ini. Nenda hospitali mtahudumiwa vizuri tu. Kwani uko wapi?
 
pOLENI SANA WAPENDWA NA MUNGU AWATIE NGUVU, PIA MSISAHAU MAOMBI WAKATI MKIENDELEA NA MATIBABU, NB: MADAKTARI WANATIBU YESU ANAPONYA. TUMIENI JINA LA YESU TU KATIKA MAOMBI YENU.
 
mbembati?! Labda ni tofauti na ninayemfahamu miye. Nendeni mnh mtahudumiwa. Mtapeleka hospital zingine wakamfanyia tapping aafu akafa. Hatuna hakika kama tatizo alilo nalo ni figo, moyo au ini. Nenda hospitali mtahudumiwa vizuri tu. Kwani uko wapi?
ahsante kwa ushauri mkuu, tupo dar mkuu
 
Poleni sana.
Kuna dr kapiteni yuko tmj hospital. Ni mzuri sana (usisikilize maneno ya watu kuwa anapenda wanawake. Mtu labda akae kikujikengesha otherwise hahangaiki na mtu).
Dr kaushik yuko hindu mandal nae naskia ni mzuri sana. Japo nahisi bill za hindu mandal ziko juu incase hana insurance card.

Kika la kheri.
 

Nenda Muhimbili, ikiwezekana ingia Fast Track utapata huduma. Mtafute Dr O. Kisanga 0784 782948 au Dr Linda 0754 290499 naamini watamsaidia mzee. Poleni sana.
 
Nenda Muhimbili, ikiwezekana ingia Fast Track utapata huduma. Mtafute Dr O. Kisanga 0784 782948 au Dr Linda 0754 290499 naamini watamsaidia mzee. Poleni sana.

Ahsante sana mkuu, tumempeleka leo asubuhi muhimbili wamemuwekea dripu wamemlaza, ila me ni mgeni kidogo pale muhimbili fast track ndio sehemu gani hapo
 
Ahsante sana mkuu, tumempeleka leo asubuhi muhimbili wamemuwekea dripu wamemlaza, ila me ni mgeni kidogo pale muhimbili fast track ndio sehemu gani hapo

Ni kama private kiasi fulani ila inakuwa hapo Muhimbili. Pia wasiliana na hao ni Madaktari Bingwa ambao wataweza kukupa msaada.Poleni sana Mkuu.
 
Kuvimba miguu na tumbo kunaweza kusababishwa na matatizo ya figo, ini au moyo.
Kama ni tatizo la figo wasiliana na Dr Kisanga yupo Renal Unit pale Muhimbili. Nitaku-PM namba yake.

Ahsante sana mkuu, ila ukinipm namba yake itakuwa vizuri zaidi mh.
 
Ni kama private kiasi fulani ila inakuwa hapo Muhimbili. Pia wasiliana na hao ni Madaktari Bingwa ambao wataweza kukupa msaada.Poleni sana Mkuu.

mkuu kwa mnh ni afadhali mgonjwa akawa changanyikeni japo kuna shida ya msongamano. Hapo atapata nafasi ya kudiscussiwa vya kutosha na vipimo vyake kufuatiliwa mapema na interns, md5, pgs kuliko ippm. Kule dr wako asipokuwepo hata inaweza pita wiki hujapitiwa. Luck enough huyo mgonjwa awe clacked na md5, utafanyiwa full investigations. I used to do so kwa wagonjwa wangu niliopresent, nilihakikisha nakuwa karibu nao na kufuatilia vipimo mpaka siku ya discharge nakuwepo. I enjoyed my school in that way, sijui kama hawa wa tcu wanafanya hivyo.
 
Siku zingine mnakuwaga watu wazuri sana. I am proud of you. Lakini siku zingine mmmmhhh sijui pepo gani huwa anawaingia!
 
Siku zingine mnakuwaga watu wazuri sana. I am proud of you. Lakini siku zingine mmmmhhh sijui pepo gani huwa anawaingia!

usisahau kuwa roho mtakavitu naye huwa anawapitia watu wake.
 
Hivi mtu akiwa na mgonjwa anampigia simu daktari au anaenda naye hospitali?

Hii ya kumpigia simu daktari wa hospitali ya umma mbona imekaa kirushwa zaidi? au ndio utaratibu wetu Tanzania?

Nakushauri nenda na mgonjwa wako katika hospitali iliyo karibu na pale ulipo ili watathmini tatizo na wakiona hawawezi kumtibia mzee watakuandikia barua ya rufaa uende kwenye hispitali kubwa kama Muhimbili. Ukienda Muhimbili bila barua ya rufaa utasumbuka bila kumjua mtu.

Ukimpigia simu daktari moja kwa moja akakupa appointment kinachotokea ni kwamba manesi na watumishi wengine wa afya wanajua daktari umemuhonga kwa hiyo jiandae kuwa nao watataka hongo. Bila hongo watajisikia kama wanamfanyia kazi huyo daktari ajiingizie pesa za hongo peke yake. Hiyo ndio perception iliyopo.

Kama mfuko wako uko vizuri nakushauri umpleke mzee Tumaini Hospital ya Upanga.
 

Nakubaliana na wewe mkuu kama mtu unamgonjwa mpeleke hospitali akapatiwe matibabu mambo ya kuanza kupigiana simu na madactari haina tija kabisa,mie namshauri ampeleke aghakhan hospital wako vizuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…