nenda kwa ras simba magomeni,usipojua kuongea na kuandika kiufasaha kimataifa anakurudishia hela yako.ada 250000 kwa 3 months na utakuwa moto wa kuotea mbali.
Kwenye mtandao kuna sehemu unaweza kukifua kiingereza chako. Nilikuwa napaste anwani ya kwenye youtube na englishbus.net lakini imeshindikana...inawezekana ndani ya JF kunakatazo.
Kwa hiyo, fungua you tube na kisha andika 'learn English speaking' utaletewa kurasa mbalimbali.
Unaweza kubadilishabadilisha mada hiyo na utajikuta umepata mengi ya kujifunza.
ALL THE BEST
Ni lazima iwe sehemu maalum au hata mtu binafsi? Umejiaandaaje kwa malipo? Naweza kukufua na ukaongea vyema. Wasiliana name kwa 0713 111171
Habari wana JF, kwenye kampuni wetu tunadili na watu wa nchi nyingi tofauti tofauti lugha kubwa inayotumika ni kiingereza, nagombana na bosi kila siku kuhusu uongeaji wangu anadai sieleweki tatizo hata sauti yangu ni ya puani na hua kama nabana maneno hata ninapoongea kiswahili.
natafuta sehemu ntakayoweza kujifunza ili kuongeza uwezo na ujasiri wa kuongea kiingereza.
Asanteni.