Msaada wa haraka wa kisheria kuhusu Sheria ya Eviction

Msaada wa haraka wa kisheria kuhusu Sheria ya Eviction

ngaiwoye

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
2,150
Reaction score
3,225
Shemeji yangu alikuwa anaishi/amepanga kwenye nyumba za shirika la uma. Kutokana na matatizo ya kiuchumi alichelewesha kodi ya pango na hivyo shirika lile likamvunjia mkataba wa upangaji na kumpa siku 14 awe ameachia nyumba. Aliandika barua kuomba aongezewe muda michache na atalipa Kodi ama atahama siku 14 ni chache sana. Hakujibiwa barua Ile Bali shirika lilielekeza kampuni ya majembe imtoe kwenye nyumba.

Siku waliyoenda kufanya eviction walikuta watoto wawili tu nyumbani, mmoja wa miaka 10 na mwingine wa miaka minne. Walimpigia simu shemeji yangu akaomba wamsubiri anafika lkn wakaendelea na zoezi na majembe walikamata Mali zote na kuzipakia kwenye Lori na shemeji yangu alipofika waliondoka na vitu vyote kwenye Lori, aliomba APEWE orodha ya vitu walivyobeba na apewe nyaraka na nguo na vyakula lkn majembe walikataa wakisema wameshapakia vitu hivyo.

Shemeji yangu aliendelea kuomba arudishiwe nyaraka hizi ambazo ni pamoja na VYETI vya taaluma pamoja na nguo zikiwemo uniform za watoto na madaftari na vitabu vyao lkn majembe walikataa kurejesha vitu hivyo walitaka alipoe storage charged. Shemeji yangu hakuwa nayo. BAADAE majembe walimwelwza kwamba wamepata majanga ya mafuriko hivyo vitu vyake vimeharibika.

VYETI vimeharibika, nguo zimeharibika na bado ni Zaid ya miaka mitano wamekataa kumrejesha VYETI hivyo pamoja na nyaraka zake muhimu ambazo zimemfanya akakosa hata ajira.

Je katika SHERIA za eviction unaruhusiwa kumkamata nyaraka, VYETI, vitambulisho na nguo na madaftari na vitabu vya WANAFUNZI?
 
Kwanza nikosa kuingia kwenye nyumba ya mtu bila idhini yake. Yan kiufupi nikwamba jamaa niwezi wamevamia nyumba ya mtu nakuiba. Kwanza ata mwenyekiti hajausishwa.Kiufupi wamefanya kienyeji sana.
 
Hao majembe ndo akina nani, ni wa hovyo sana.!! hawana Locus standi ya kufanya kitu kama iko.

Atafute mwanasheria wakafile case ya jinai na madai sheria ifuate mkondo
 
Shemeji Saiv analala wap na analula wap?,Nataka Nisaidie Majukumu ya Basic Needs na kwa watoto
 
Kwanza nikosa kuingia kwenye nyumba ya mtu bila idhini yake. Yan kiufupi nikwamba jamaa niwezi wamevamia nyumba ya mtu nakuiba. Kwanza ata mwenyekiti hajausishwa.Kiufupi wamefanya kienyeji sana.
Walikuwa wapo na mtendaji wa mtaa na nyumbani walikuta watoto wadogo..mtendaji MLA rushwa sababu Mali haxikuorodheshwa...lkn SWALI tunalouliza je ni halali wao kushikilia nyaraka za muhimu kama VYETI, madaftari vitabu uniform??
 
Dawa y kodi ni kulipa tu!! Au kuhama nyumba ya wenyewe.

Kazi ni kipimo cha UTU
Sawa shemeji anaelewa Hilo na aliandika barua ya kupewa muda kidogo alipe. Sema nafkiri Kuna mtu aliitaka hiyo nyumba kwani ni ya shirika..
Je kushikilia vyeti vya taaluma na nyaraka na madaftari vitabu nguo ni halali?..
 
Sawa shemeji anaelewa Hilo na aliandika barua ya kupewa muda kidogo alipe. Sema nafkiri Kuna mtu aliitaka hiyo nyumba kwani ni ya shirika..
Je kushikilia vyeti vya taaluma na nyaraka na madaftari vitabu nguo ni halali?..
pengine wakati wanachukua vitu vya shemeji yako isingekuwa rahisi kufahamu ndani yake kuna vyeti au madaftari ya shule,ila kwa namna yoyote ile zoezi la kuchukua vitu halikufanyika kwa haki au usawa kama ulivoeleza hapo awali.
 
Shemeji yangu aliendelea kuomba arudishiwe nyaraka hizi ambazo ni pamoja na VYETI vya taaluma pamoja na nguo zikiwemo uniform za watoto na madaftari na vitabu vyao lkn majembe walikataa kurejesha vitu hivyo walitaka alipoe storage charged. Shemeji yangu hakuwa nayo. BAADAE majembe walimwelwza kwamba wamepata majanga ya mafuriko hivyo vitu vyake vimeharibika.

VYETI vimeharibika, nguo zimeharibika na bado ni Zaid ya miaka mitano wamekataa kumrejesha VYETI hivyo pamoja na nyaraka zake muhimu ambazo zimemfanya akakosa hata ajira.
nafikiri badala ya shemeji yako kuendelea kusubiri kupata fidia au stahiki yoyote kutoka kwa brokers,anaweza kuanza kufanya uataribu kwenda katiika Taasisi husika za Elimu ya kupatiwa Vyeti vingine vya taaluma ili asiendelee kupoteza nafasi zingine za kazi au ajira kama ulivyoeleza
 
japo ni vyema pia kuapata msaada wa Wakili/Mwanasheria ambaye atakuongoza kwa ukamilifu zaidi,pia ntarudi hivi punde kutoa mawazo yangu juu ya hilo
 
Shemeji yangu alikuwa anaishi/amepanga kwenye nyumba za shirika la uma. Kutokana na matatizo ya kiuchumi alichelewesha kodi ya pango na hivyo shirika lile likamvunjia mkataba wa upangaji na kumpa siku 14 awe ameachia nyumba. Aliandika barua kuomba aongezewe muda michache na atalipa Kodi ama atahama siku 14 ni chache sana. Hakujibiwa barua Ile Bali shirika lilielekeza kampuni ya majembe imtoe kwenye nyumba.

Siku waliyoenda kufanya eviction walikuta watoto wawili tu nyumbani, mmoja wa miaka 10 na mwingine wa miaka minne. Walimpigia simu shemeji yangu akaomba wamsubiri anafika lkn wakaendelea na zoezi na majembe walikamata Mali zote na kuzipakia kwenye Lori na shemeji yangu alipofika waliondoka na vitu vyote kwenye Lori, aliomba APEWE orodha ya vitu walivyobeba na apewe nyaraka na nguo na vyakula lkn majembe walikataa wakisema wameshapakia vitu hivyo.

Shemeji yangu aliendelea kuomba arudishiwe nyaraka hizi ambazo ni pamoja na VYETI vya taaluma pamoja na nguo zikiwemo uniform za watoto na madaftari na vitabu vyao lkn majembe walikataa kurejesha vitu hivyo walitaka alipoe storage charged. Shemeji yangu hakuwa nayo. BAADAE majembe walimwelwza kwamba wamepata majanga ya mafuriko hivyo vitu vyake vimeharibika.
1. pale ambapo mkataba wa Upangishaji unapokwisha muda wake(Malipo)basi moja kwa moja mpangaji anapoteza haki ya yeye kuwa mpangaji katika jengo au nyumba husika na kwa mjibu wa sheria anachukuliwa kama Mvamizi(Trespasser),na akishapewa Notisi na Mwenye nyumba ya Kuhama au kuhlipa kodi katika muda aliojulishwa basi Mwenye Nyumba anayohaki ya kutumia njia yeyote ile ya kumtoa katika nyumba yake ikiwemo kutumia madalali(Court Brokers) au kufungua kesi katika Baraza la Ardhi dhidi ya mwamizi(Trespasser) ambaye alikuwa mpangaji wake,kwa sababu mpangaji alishindwa kuhama mwenye kwa hiara yake hivyo kumfanya mwenye nyumba kulazimika kutumia nguvu kumtoa.

2.Mtu yeyote ampaye alipata madhara ya eviction kwa namna yoyote ile hana haki ya kisheria ya kupata fidia yoyote kutoka kwa aliyekuwa mwenye nyumba yake wala kwa Court broker kwani Mvamizi/Trespasser,sabbu ya hivyo ni kuwa sheria umempa kila mtu haki ya kutumia na kudarhia mali yake pasipo kuingiliwa au kuadhiriwa na mtu yeyote na katika kuhakikisha haki hiyo haivunjwi na yeyote basi anaweza kutumia namna sahihi za kuzuia uvunjifu wa yeye kutumia haki yake,pamoja na hayo katika sheria kuna kanuni ambayo inasema that no person should be allowed to benefit from his own wrong -"Nullus Commodum Capere Protect De Injuria Sua Propria."
 

Attachments

1. pale ambapo mkataba wa Upangishaji unapokwisha muda wake(Malipo)basi moja kwa moja mpangaji anapoteza haki ya yeye kuwa mpangaji katika jengo au nyumba husika na kwa mjibu wa sheria anachukuliwa kama Mvamizi(Trespasser),na akishapewa Notisi na Mwenye nyumba ya Kuhama au kuhlipa kodi katika muda aliojulishwa basi Mwenye Nyumba anayohaki ya kutumia njia yeyote ile ya kumtoa katika nyumba yake ikiwemo kutumia madalali(Court Brokers) au kufungua kesi katika Baraza la Ardhi dhidi ya mwamizi(Trespasser) ambaye alikuwa mpangaji wake,kwa sababu mpangaji alishindwa kuhama mwenye kwa hiara yake hivyo kumfanya mwenye nyumba kulazimika kutumia nguvu kumtoa.

2.Mtu yeyote ampaye alipata madhara ya eviction kwa namna yoyote ile hana haki ya kisheria ya kupata fidia yoyote kutoka kwa aliyekuwa mwenye nyumba yake wala kwa Court broker kwani Mvamizi/Trespasser,sabbu ya hivyo ni kuwa sheria umempa kila mtu haki ya kutumia na kudarhia mali yake pasipo kuingiliwa au kuadhiriwa na mtu yeyote na katika kuhakikisha haki hiyo haivunjwi na yeyote basi anaweza kutumia namna sahihi za kuzuia uvunjifu wa yeye kutumia haki yake,pamoja na hayo katika sheria kuna kanuni ambayo inasema that no person should be allowed to benefit from his own wrong -"Nullus Commodum Capere Protect De Injuria Sua Propria."
Minimum Notice ni siku 30 counsel, andika polepole
 
Back
Top Bottom