Msaada wa Imani

Hapo ndipo njia zinapopishana ndugu. Sisi waislamu tunaamini Mungu ni muweza wa kila Jambo. Ikiwemo la kukusamehe wewe Dhambi zako. Yaani kwa kifupi hana haja ya Kujibadili awe mwanadamu halafu Afe ndio yeye tena huyo huyo aliokufa atusamehe? Whats the point kufa then kufufuka? Ndio maana nikasema Mungu si Kama wachawi wa kutaka Kafara fulani ya Damu ya Mtu ili Jambo litimie!
Yaani kwa kifupi haiwezekani Mungu kushindwa kuWasamehe watu aliowaumba Yeye mwenyewe mpaka Amwage Damu ?
Anyways kwa uelewa wangu watu wengi wakienda kuungama Dhambi makanisani mchungaji anawaambia Nenda Umesamehewa! Je mchungaji ana nguvu kuliko Mungu?
 
Asante kwa kujibu kadri ya uelewa wako. Nami naomba nikuulize swali moja. YESU ALIPOKUA MSALABANI alilia ELOI ELOI MUNGU WANGU MUNGU WANGU. alikua anamlilia nani? Na Huyo Mungu wake Yesu ni Nani?
 
Yesu ni Mungu na mtu. " alikufa 14/01/31 AD saa Tisa alasiri siku ya ijumaa.
 
Yesu ni Mungu na mtu. " alikufa 14/01/31 AD saa Tisa alasiri siku ya ijumaa.
Kipindi anakufa alikua anamlilia nani? Na ni nani alietoa uhai wake? Na kabla ya kifufuka yaani wakati kafa nani alikua anaendesha Dunia? Maana hilo ndilo lingekua gepu la shetani kushika usukani [emoji23] . Na ni nani aliemfufua siku ya Tatu?
 
Huu utata wa Yesu ni Mungu au sio Mungu ni wazi kuwa biblia ina tatizo,kwa sababu hili si tatizo la kutofautiana uelewa tu wa kutafsiri maandiko bali maandiko yenyewe pia huchanganya watu.

Hivyo huu ubishi unatia mashaka usahihi wa biblia.
 
Huu utata wa Yesu ni Mungu au sio Mungu ni wazi kuwa biblia ina tatizo,kwa sababu hili si tatizo la kutofautiana uelewa tu wa kutafsiri maandiko bali maandiko yenyewe pia huchanganya watu.

Hivyo huu ubishi unatia mashaka usahihi wa biblia.
Leo nimekudaka mkuu.... naona kwa atheist unaponda, kwa wakristo unaponda, kwa waislamu unaponda, kwa agnostic unaponda. Who are you????
Umekuwa non aligned.... u want people to be free, they should not be questioned? yaani set yako ni ngumu kutambulika mkuu.
 
Kuponda maana yake nini?
 
Asante kwa kujibu kadri ya uelewa wako. Nami naomba nikuulize swali moja. YESU ALIPOKUA MSALABANI alilia ELOI ELOI MUNGU WANGU MUNGU WANGU. alikua anamlilia nani? Na Huyo Mungu wake Yesu ni Nani?

Ninaamini katika utatu Mtakatifu,MUNGU baba,MUNGU mwana na Roho mtakatifu.Swali la kuhoji uungu wa Yesu Kristo haliishi hapo tu unapotumia akili zako mwenyewe.Nitakupa nyongeza ya maswali.Yesu pia alisema naenda kwa Baba kuwaandalia makao ili mimi nilipo nanyi muwepo.Waweza kuhoji kama alikuwa MUNGU kwa nini alisema nakwenda kwa baba?

Alipoulizwa siku ya mwisho pia jibu lake litakupa maswali.Alipoulizwa ni lini mwisho wa ulimwengu alitoa ishara na akasema kwa habari ya siku na saa si malaika wala mwana ajuaye.

Hoja hizi hazimuondoei Yesu Kristo Uungu wake.Kwa kuwa wahoji nami nitakuuliza.Je waiamini Biblia? Kama waiamini tuendelee kujadiliana ,kama waamini kuwa imejaa uongo nitakuwa nakupotezea muda.

Kama unaiamini je umewahi kujiuliza ni kwa nini wana wa Israel walipokuwa njiani na kukutana na mashambulizi ya nyoka dawa ilikuwa kumwangalia nyoka wa Shaba na kupona na waliopuuza kumwangalia wakafa?

Je ni kitu gani kilisababisha Musa kuamriwa kupiga maji kwa fimbo tu ili kuwapa wana Israel maji walipolalamika kiu kwa kukosa maji?

Kwa nini Yesu alimwambia mwanamke Msamaria katika kisima cha Yakobo" laiti ungelijua ungeniomba maji yaliyo hai"

Kwa wasioamini kuwa Yesu ni MUNGU wala si mwana wa MUNGU wanaweza kuyauliza mapepo yalipomwona tu yakaanza kujitetea" tuna nini nawe ee mwana wa MUNGU" Je wajua asili ya kuwepo mapepo? wajua yalifikaje Duniani?

Je waamini habari ya kiama na kufufuka kwa wafu? kama waamini niambie kwa mujibu wa Imani yako nani atakayewahukumu walio hai na wafu?

Jambo la muhimu si kujua kama Yesu ni MUNGU,Mwana wa MUNGU au mtume.Muhimu ni kuamini moyoni mwako kuwa alikufa kwa ajili yetu yaani mimi na wewe, kumkiri kwa kinywa chako kuwa MUNGU alimfufua katika wafu na siku ya mwisho atauhukumu Ulimwengi.
 

Jaffar;
Nashukuru kuwa umeeleza uelewa wako kuhusu msamaha. Sawa kabisa kama ulivyosema kuwa ninyi waislamu mnaelewa kuwa Mungu anaweza kila kitu. Sasa, unaposema kuwa huoni mantiki ya Mungu kuimwaga damu ya Nafsi yake yeye mwenyewe ili kawa damu hiyo auokoe ulimwengu hapo ndipo umeniacha hoi.
Ati Mungu mwenye uwezo, asiyehitaji ushauri, tumwulize kwa nini kaimwaga damu yake mwenyewe ili atukomboe. Nasema Haikuji!! Atakuwa si Mungu tena anapoulizwa na alichokiumba kuwa kwa nini ulinifanyia hivi??. Nasema haikuji.
Jaffar, Naomba Amini kuwa hakuna aliyewahi kumkosoa Mungu wala Mungu hakosei. Alichofanya kafanya kwa; Mapenzi yake, Namna yake, Njia zake. Uu nani weye unaye muuliza kwa nini ulifanya hivi?? Jaffar, Amini tu ka mtoto mchanga. Swali si kwa nini Yesu Kristo alikufa bali alimfia nani. Alikufia weye ili kwa dhabihu ya damu (Uhai) wake weye uwe mzima.
Kwa nini mtu huchukua maharage mazuri yasiyo na doa, akaenda kuotesha gunia zima kipindi cha njaa kwa sababu tu kaona mvua?? Hujiulizi hilo?? Kama sisi tuna ujasitiri huo. Mungu naye kwa ujasiri akamtoa mwana wa pendo lake (Nafsi yake halisi) Afe, azikwe, afufuke katika upya wa uzima, kukuonesha weye kuwa, Japo ulikufa katika dhambi, ukimwamini, atakupa uzima mpya.
Huo uelewa wako wa wanaowasamehe watu dhambi; Si kila mchungaji husema hayo. Nachojua ni kwamba; Dhambi ni makosa. Ukiomba msamaha kwa mtu ambaye hujamkosea, una tatizo. Mimi huungama kwa Mungu wangu, nilimkosea yeye wala sio mtu mwingine. Nitamuungamia Mungu peke yake wala sihitaji mtu wa kunisaidia kuomba msamaha.
 
Vizuri kabisa Yesu alisema anakwenda kwa Mungu wake ambae ni Mungu wetu. Na Naenda kwa Baba yake ambae Ni Baba Yetu. Sasa je Unataka kusema alikua anadanganya na unataka kubadili maandiko na kumuita yeye ni baba? Hali ya kua ameshakiri Yeye mwenyewe mara Nyingi kua Baba yake ni Mkuu kuliko yeye?

pia umeongelea suala ya Yesu kutokujua siku ya hukumu itakua lini? Je unaamini kabisa Mungu ana sifa ya kutokujua jambo?
na Yesu sio tu hajui siku wala saa, pia hakujua hata mti kama una matunda au hauna.

kuhusu suala la kuiamini biblia nadhani ni vyema kwanza nikifahamu kama wewe unaamini kua maneno yote ya kwenye Biblia ni sahihi na kama unaamini biblia haijatiwa mikono ya waandishi. Nijibu hili ili tuendelee
 
K

Kaka nimekujibu na kukupa maswali ya nyongeza ya kitu kile kile.Nawe nijibu.Je waiamini Biblia? Je waamini kiama? Nani ataikumu Dunia? ukijibu nitaendela usipojibu nitanyamaza.Lililomu nimekujulisha una hiari ya kukubali au kukataa.
 
Hebu nikupe mfano mdogo ili uelewe ulichokisema hapo juu. hili si suala la kukubali tu kulielewa kama mtoto mdogo. maana mara nyingi watoto wadogo hua wanadanganywa mambo mengi. Kama mtoto akiuliza sisi tunazaliwaje? Utamwambia kitendo kilichofanyika? Kuna wakati mtoto atauliza mbona baba anamkia na mama hana? Utajibuje hapo? [emoji23]
Haya utani tuweke pembeni

Tuchukulie Wewe ni hakimu na unamwanao anaitwa James. Unampenda sana mwanao kuliko chochote hapa duniani. Mara anakuja Bw.Yuda mahakamani. Mashtaka yake ni haya, yeye ni mzinzi, mnafiki, analawiti watoto n.k. na wewe kama hakimu una mamlaka yote kabisa. Yaani unaweza kuhukumu auwawe, ama pia unaweza kumsamehe na kumuacha huru. Kwa kifupi unauwezo wa kutoa adhabu uipendayo..sasa wewe unasema Bw. YUDA nakupenda sana. HIVYO unaamrisha Maaskari wamkamate Mtoto wako kipenzi JAMES na WAMUUE ili uweze KUMUACHA huru BW[emoji830]YUDA. MTOTO WAKO ANALIA MACHOZI na kusema Baba mimi sina kosa. Unasema ndio lakini nampenda Sana BW.YUDA hivyo LAZIMA UFE TU!!

HICHO NDICHO unachotaka kiaminike kweli?

Pili naomba nijue msimamo wako kuhusu Yesu kabla ya Kuendelea. Je unamwamini kama nani? MJUMBE WA MUNGU? MUNGU MWENYEWE? MWANA? ama Mwokozi?
 
K


Kaka nimekujibu na kukupa maswali ya nyongeza ya kitu kile kile.Nawe nijibu.Je waiamini Biblia? Je waamini kiama? Nani ataikumu Dunia? ukijibu nitaendela usipojibu nitanyamaza.Lililomu nimekujulisha una hiari ya kukubali au kukataa.
Sijaona jibu ndio maana nimeuliza yangu pia.
Nikujibu kwa swali je wewe unaiamoni biblia? Unaamini biblia ni neno la Mungu? Na je unaamini kua biblia haibadilishwa ama kutiwa kalamu za waandishi?

Kuhusu kiama nakiamini ndio

Kuhusu suala la nani atahukumu jibu ni Mungu mwenyewe ndio atahukumu dunia kutokana na matendo yetu ya hapa duniani ni si kutokana na Kuamini fulani alikufa kwa ajili ya dhambi zetu.

Swali kubwa ambalo nategemea ulijibu ni kuhusu Biblia pale juu.
 
Hii ni ngumu kumeza sio siri.

Mungu akaandaa mpango wa kuwakutanisha binadamu na Mungu........
Nahisi sina roho mtakatifu ndio maana siwezi kuelewa hiki kipengele.
1Yohana 5:8-9
8: Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja.
9: Kisha wako watatu washuhudiao duniani], Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa habari moja.....

"Nahisi hiyo itakusadia kumeza vizuri"
 

Jaffar;
Nimeshakueleza mara kadhaa, unapo mlinganisha Mungu Muumba wa vyote na alichokiumba una shida. Mungu hakuja kuuhukumu ulimwengu bali kuuponya ulimwengu. Kulikuwa hakujawepo mpango mwingine ka huu hivyo mfano wako wa mwanagu James na labda nimwite jirani Yuda haviko hivyo!!
Ukombozi wa Mungu kwa ulimwengu ni tofauti. Tunasoma hivi; Yoh. 3 : 16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanaye pekee, ili kila mtua amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. 17 Maana Mungu hakumtuma Mwanaye ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe kwa yeye. 18 Amwaminiye yeye (Huyo Mwana) hahukumiwi; asiyemwamini (Huyo Mwana pekee) amekwisha hukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
Jaffar, Kwa nini tunataka kumfundisha Mungu?? Tulimkosea sisi, halafu tunataka atusamehe tunavyotaka sisi wala si kama atakavyo yeye. Huku tunajitia nguvu kuwa Mungu wetu aweza kufanya lolote. Kuna kasoro mahali fulani. Huenda tunajifanya vipofu na viziwi wenyewe.
Angalia Yoh. 3 : 19
Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru ilikuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.

Amini kuwa ulimkosea Mungu na ni yeye Mungu tu awezaye kukusamehe. Tiyari kisha kusamehe, amini tu.
 

Naiamini Biblia kuliko kitabu kingine chochote,
 
Mkuu haya maandiko hawapewi watu wanafiki wanapewa wajinga.

Usiwe mwepesi mara zote kutoa andiko.

Hawa wanajibiwa kwa kutumia vichwa vyao wenyewe.
 
Habari wana JF. naomba kufahamishwa kuhusu Yesu Mtoto wa Mariam. Je Imani ya Wasabato, Waroma na Madhehebu mengine wanamchukulia kama Nani? Je ni Mungu? Mwana wa Mungu ama Mtume wa Mungu? Asanteni.
Achana nae fanya mambo mengne. Utapasuka kichwa.
Uislam kaja nao mwarabu na sijui aliutoa wap???
Ukristo kaja nao mzungu. Sijui na yeye aliuokota wap.

Lakin yote hayo mapazia ya kubeba vito vya saman. Sasa wwe jichanganye kuuliza maswal ya kipuuz wakat hakuna aliyekufa akafufuka kuja kuleta aliyoyaona huko. AMIN MUNGU BASI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…