Msaada wa kisaikolojia

Msaada wa kisaikolojia

Averos

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2010
Posts
993
Reaction score
703
Wanajamvi, naomba mnisaidie ni kitu gani kinatengeneza tabia ya mtu, yaani mwngine anakuwa mkali, mwengine mpole, mwengine bahili, mwengine mpenda makuu, mwengine mchafu, mwenigne mtanashat, mwengine katili, mwengine mlafi, mchoyo, mroho, na tabia nyenginezo kama uwongo, ukweli, umbea na kadhalika.
 
Wanajamvi naomba msaada wa kujua sababu ya binadamu kuwa na tabia mbalimbali kama uvivu, ukarimu, ushujaa, umbea, upole, ukali, uwongo, kupenda sifa na kadhalika.
 
binadamu ni kama wanyama wengine tu, kuna tabia za kurithi (za kuzaliwa nazo) na kuna tabia za kufunzwa, na ndio maana si ajabu una kuta watoto wa familia moja waliolelewa malezi ya wazazi wamoja lakini wanatofautiana kitabia
 
Tabia hizo hurithiwa na zingine hutokana na mazingira unayoishia. Pia tabia zingine hutegemea context kwa mfano, namna nitakavyobehave nikiwa kwenye nyumba ya ibada ni tofauti na namna nitakavyobehave nikiwa club.
Kwahiyo hapo ni sababu 3. Wengine watajazia.
 
Kabala ya kugusia nini chanzo za tabia tulizo nazo ningependa nitoe maana fupi ya tabia: Tabia ni jumla ya matendo yote ayafanyayo mtu ama mnyama. Mambo haya yanajumuisha yale tunayoyaona kwa macho (mfano kula, kulala, kunywa, kutembea, kukonyeza, kuua, kuiba, kupigana, kusoma, nk) na yale tusiyoyaona kwa macho, mfano kufikiri, hisia zetu nk. Mambo makubwa mawili yanayofanya tuwe na tabia tulizo nazo

1. Urithi kutoka kwa wazazi wetu kibailojia.

2. Mazingira. Unapozungumzia mazingira unaangalia mambo mengi, mfano, watu wanaotuzunguka. Mtu anaweza akaiga tabia za mtu mwingine, misukumo (pressure) kutoka kwa watu wangu, malezi, ugumu wa mazingira tunamoishi, kiwango cha elimu nk. Kwa ujumla mazingira ni mambo yote ambayo sio ya kibaiolojia.

Hope imekupa mwanga.
 
Back
Top Bottom