Msaada wa kisaikolojia

Halafu naona kama umeamua kulikumbatia tatizo na kujisemea siwezi kusamehe jifunze kuachilia mambo maana naona kama unajitesa na unatesa watoto wa watu
Hiyo nguvu ya mabadiliko ipo kwako mwenyewe wewe ndiye mwenye maamuzi ya kujikomboa kutoka katika hiyo hali kwa kuachilia yaliyopita na kusongambele .Mungu anahitaji kushirikishwa katika hili
 

lin ni vyema lakini pia yeye anahitaji kujifanyia councelling na kuikataa hali kwasababu hata akifanyiwa na mtu na bado hayupo tayari kuachilia bado atakuwa kwenye kifungo mambo mengine yanaanza na wewe wenyewe kwanza .Sasa kila kitu anasema siwezi siwezi unafikiri mengine yatawezekanaje? mamy?
 

nakubaliana na wewe 100% mtu binafsi asipokubali kuliachilia jambo akaendelea kulibeba moyoni hata asaidiwe vipi tatizo litabaki palepale
 
Kwanini unakuwa na mtazamo hasi kwanini unaamnini hakuna atakaye kuelewa ? Je ni kwasababu ya unawamistreat?
Kataa hiyo hali acha kumtukuza ibilisi

Nataka lakini hakuna anayenielewa licha ya kuwa wazi.
 
nakubaliana na wewe 100% mtu binafsi asipokubali kuliachilia jambo akaendelea kulibeba moyoni hata asaidiwe vipi tatizo litabaki palepale

Sijasema kwamba siwezi, naweza na ndio maana nikaamua kuusemea moyo baada ya kujitathimini kwa kina na kutambua tatizo so nataka pa kuendelea kuivua hali hii.
 
Pole sana mkuu kwa bahati mbaya sipo Tz kwasasa ila niPM nikuonganishe kwa Psychologists wenzangu na nikupatie no zao
Ahsante
 
Mmmh! Mkuu kama hisia za midadi unazo hata usijilazimishe kupenda! Ni mateso sana kumpenda mtu hata kama unalala naye!

Unachotakiwa kufanya ni kuwa muadilifu, kutona na maelezo yako ni kuwa hauna mapenzi na hauna uadilifu!

Ukumbuke, mapenzi na uadilifu ni vitu viwili tofauti ingawa vinashabihiana!
Unaweza kupenda na usiwe muadilifu!
Unaweza kuwa muadilifu na usipende!
Unaweza kuwa muadilifu na ukapenda na unaweza kuwa usipende na usiwe muadilifu (na hii ndio hali uliyonayo!)

Kuna article moja nilisoma inasema ukitaka maendeleo tazama mbele! Ukiangalia nyuma hautaweza kutembea vizuri, aidha unaweza kujikwaa na kuvunjika!

Ile article ilitolea mfano wa mtu anaepanda mti mrefu, ilisema: ukiangalia chini unaweza usipande tena kwa sababu utajipangia mahesabu ya kudondoka na athari zake, kitendo cha kufikiria hivyo tu unajijengea disorder inayoitwa anxiety!

Alafu jaribu kumsoma huyu mtaalamu (Sigmund Fraud) unaweza ukapata kitu humo!

Id, Ego and Superego - Structural Model of Personality
 

Asante sana ndugu
 
Pole sana ndugu! Hii hali unaweza kufanikiwa kuitatua endapo utapata ushauri wa Kisaikolojia na tiba kwa muda mrefu (psychotherapy) ambayo itasaidia kubadili mtazamo wako. Wataalam wa mambo ya akili wanapatikana hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kitengo cha magonjwa ya akili. Waone hao watakusaidia kurudi kwenye hali yako nzuri ya afya ya akili.
 
Sijasema kwamba siwezi, naweza na ndio maana nikaamua kuusemea moyo baada ya kujitathimini kwa kina na kutambua tatizo so nataka pa kuendelea kuivua hali hii.

nimekupata allan,amin hilo tatizo litaisha tu coz kutambua tatizo ulilonalo tayari ni nusu ya utatuzi wake
 

Nashukuru ndugu yangu
 
Kwanini unakuwa na mtazamo hasi kwanini unaamnini hakuna atakaye kuelewa ? Je ni kwasababu ya unawamistreat?
Kataa hiyo hali acha kumtukuza ibilisi

Kila unayemueleza anasepa au anaamini namake up a story na mazingira ya kumkimbia. So mtu asipo nielewa inaniuzi sana
 
Kila unayemueleza anasepa au anaamini namake up a story na mazingira ya kumkimbia. So mtu asipo nielewa inaniuzi sana
Tune yourself jikubali kuwa wewe ni mwanaume kamili ambaye anapaswa kuwa na mwanamke na ukamfanya mwanamke awe proud na wewe usimuundermine mwanamke kwa kuangalia mambo ambayo wengine wamekutendea.
Halafu no need to tell a person your problems at first unaweza kuwa nae kwenye mahusiano baadae ukamweleza kama story tuu. hakuna haja ya kwenda kwa counceller wewe ni counceller namba moja
 

Hapo nimekupata vyema Gemmy. Wacha nianzie hapo. Nashukuru kwa kuustua moyo wangu kwa mbaaali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…