Msaada wa kisheria juu ya matunzo kwa mtoto asie wa ndoa

Msaada wa kisheria juu ya matunzo kwa mtoto asie wa ndoa

Nina ujauzito wa mtu ambae baada ya kugundua nina ujauzito akaanza visa vya kunikwepa na kunikana.
Sasa naona anataka anitelekeze na kuniachia majukumu mwenyewe. Amesema nijifungue kisha tutaongea na kuna muda hataki kabisa kugusia hilo swala.Ujauzito ni wa miezi mitano.
Nilikua na ndoa ila tulitengana ndipo nikajikuta niko na huyu bwana,
Je nikijifungua haki za mwanangu ni zipi? Niko tayari kupima vinasaba ili ajihakikishie kua yeye ndie mzazi wa mtoto atakae zaliwa maana kuna wakati alianza kuleta maneno kua haniamini.
Kikubwa ninachohitaji ni matunzo kamilifu kwa mtoto.
Naomba msaada juu ya hili.
Pole sana aisee, kama huyo mtu anaroho ya kibinadamu atamtunza vizuri mtoto wake, ila kama akili zake fyatu sheria haina msaada sana, bado iko kikandamizi zaidi kwa wanawake,kiasi atakachopaswa kutoa ni kidogo sana kulinganisha na hali halisi, kiufupi sheria haijatambua bado thamani ya muda ule ambao utakua unautumia kulea mtoto huku aliyekupa mimba akiendelea na majukumu yake ya kiuchumi lakini sheria inasema matunzo ni asilimia 50 kwa 50, huwa nawachukia sana wanaume wanaokimbia majukumu yao ya malezi kwa watoto.
 
Kulea mtoto ni wajibu wa wazazi ndio maana hata wengi walikubali (hata kwa shingo upande) yale mashauri ya kwa Mkuu wa mkoa wa D'salaam.
 
Jiandae kulea huyo mtoto peke yako mkuu, maana hapo hana uhakika.

Kakuambia kuwa ukijifungua mtaongea ili ukizaa apate uhakika kama ni wake
 
Shukrani Baraza, ningefurahi karma mngejibu bila jazba wala hasira.Maana swali limeandikwa bila hasira. Maoni yenu woteeee ni muhimu na yanazingatiwa sana.
By the way mwenzenu ni mwanafunzi wa LAW SCHOOL ila nimeuliza hapa jukwaani kwa makusudi maalum. Wasalaam
 
Shukrani Baraza, ningefurahi karma mngejibu bila jazba wala hasira.Maana swali limeandikwa bila hasira. Maoni yenu woteeee ni muhimu na yanazingatiwa sana.
By the way mwenzenu ni mwanafunzi wa LAW SCHOOL ila nimeuliza hapa jukwaani kwa makusudi maalum. Wasalaam
So huna mimba ila ulikuwa unatuchora
 
Back
Top Bottom