mwl.lukiko
Member
- May 2, 2013
- 26
- 7
Salaamz,
Yupo mama kaniomba ushauri juu ya ndoa yake, nami nimeona suala limekaa
kisheria zaidi, hivyo naomba ushauri/msaada wa nini kifanyke. Mama huyu
ana mgogoro wa ndoa yeye na mmewake(hawajatengana), mwanaume kaamua
kuokota kabinti mtaani anatembea nako. Imefika mahali huyo mzee kaanza
kuuza mali alizochuma pamoja na mke wake wa ndoa na kwenda kutumbua na
mke wake mpya. je sheria inasema nini juu ya jambo hili, mke anahaki ya
kwenda mahakamani kupinga uuzwaji wa nyumaba ? na je mume ana mamalaka
kisheria kuuza mali yoyote waliyochuma na mkewake pasi kumshirikisha
mkewe. kama inatokea hivyo hatua gani zichukuliwe kwa mke kupata haki
yake. je kuna vituo vya msaada wa kisheria vya kuweza kumsaidia huyu
mama..? muongozo tafadhali...asanteni..
kwanza aende aka-file caveat mahakaman kuzuia mali zilizobaki, pili afungue kesi kupinga uuzwaji wa mali bali her consent. kesi simple hii kitarudi kila kitu hata aliyenunua itakula kwake