Roga Roga
JF-Expert Member
- Dec 20, 2013
- 656
- 499
Ndugu wadau wa Jf naomba mniweke sawa hasa katika masuala ya kisheria kwa mtumishi wa uma anapopata matatizo ya kiafya akiwa kazini.
Nina mdogo wangu ameajiriwa halimashauri ya Masasi, Mtwara, tangu mwaka jana mwishoni amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya, ametibiwa huko Masasi bila mafanikio na kupewa rufaa kuja hospitali ya mkoa ya Ligula mtwara. Hapa hospitali ya rufaa bado hakupata nafuu yoyote na hivyo kupewa rufaa kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili kwaajiri ya uchunguzi zaidi.
Tangu akiwa Masasi baadae kuja mtwara na kuelekea hospitali ya Muhimbili hakuna msaada wowote wa kifedha kwaajiri ya safari,chakula na pakulala ameupata toka kwa mkurugenzi wa masasi ambaye ni muajiri wake. Muda aliotumia Muhimbili ni mwezi mmoja na nusu. Baada ya kupata nafuu, amerejea kazini tangu mwezi march mwaka huu na pia akachukua jukumu la kuomba arudishiwe gharama zote alizotumia katika matibabu ikiwemo safari,chakula na gesti.
Pia kama mjuavyo hospitali nyingi za serikali hazina vipimo vya kueleweka,na wakati mwingine ilimlazimu kutumia fedha yake kwenda kufanya vipimo katika hospitali binafsi ili kuokoa maisha yake. Viambata vyote vya tiketi, matibabu,vipimo amewasilisha lakini mpaka leo hajarudishiwa gharama hizo. Je ni sheria ipi ya kazi inaweza kumlinda na hatimaye kufidiwa? Ikumbukwe matatizo yake yamepatikana akiwa kazini? Na sasa baada ya kufatilia muda mrefu wanamtishia kumfuta kazi.
Msaada wenu ni muhimu.
Nina mdogo wangu ameajiriwa halimashauri ya Masasi, Mtwara, tangu mwaka jana mwishoni amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya, ametibiwa huko Masasi bila mafanikio na kupewa rufaa kuja hospitali ya mkoa ya Ligula mtwara. Hapa hospitali ya rufaa bado hakupata nafuu yoyote na hivyo kupewa rufaa kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili kwaajiri ya uchunguzi zaidi.
Tangu akiwa Masasi baadae kuja mtwara na kuelekea hospitali ya Muhimbili hakuna msaada wowote wa kifedha kwaajiri ya safari,chakula na pakulala ameupata toka kwa mkurugenzi wa masasi ambaye ni muajiri wake. Muda aliotumia Muhimbili ni mwezi mmoja na nusu. Baada ya kupata nafuu, amerejea kazini tangu mwezi march mwaka huu na pia akachukua jukumu la kuomba arudishiwe gharama zote alizotumia katika matibabu ikiwemo safari,chakula na gesti.
Pia kama mjuavyo hospitali nyingi za serikali hazina vipimo vya kueleweka,na wakati mwingine ilimlazimu kutumia fedha yake kwenda kufanya vipimo katika hospitali binafsi ili kuokoa maisha yake. Viambata vyote vya tiketi, matibabu,vipimo amewasilisha lakini mpaka leo hajarudishiwa gharama hizo. Je ni sheria ipi ya kazi inaweza kumlinda na hatimaye kufidiwa? Ikumbukwe matatizo yake yamepatikana akiwa kazini? Na sasa baada ya kufatilia muda mrefu wanamtishia kumfuta kazi.
Msaada wenu ni muhimu.