Msaada wa kisheria kwenye kesi ya Mirathi

Msaada wa kisheria kwenye kesi ya Mirathi

jokielias

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2013
Posts
1,203
Reaction score
359
Kuna Professa Mmoja (Jina namhifadhi) ambaye alifariki Dunia 2012. Kaacha Majanga kwa watoto wake kwa Sababu hakuandika wosia kabisa. Huyo Mzee tumsamehe tu lakini nachoomba ni ushauri tu kwa wataalamu wa Sheria.

Huyu Professa alioa mwaka 1984 na mke wa kwanza ni mzungu na akazaa naye watoto wawili.(Mtoto Wa kwanza ni wa kiume wa na Mtoto wa pili ni wa kike) na waliishi hapa Dar na Wakajenga Nyumba Mikocheni na kununua Magari na Kiwanja. Sasa kwenye miaka 1990 walipeana talaka na waliachana na huyu Mzungu mwanamke akarudi kwao ulaya.
Professa alibaki dar na mali zote pamoja na watoto wake na aliwasomesha watoto wake hadi elimu ya chuo.

Sasa huyu professa alikuja kuoa tena mwanamke mwingine 2005 na alizaa naye Mtoto mmoja wa kike. Huyo Professa alinunua kiwanja na alimjengea mke wake wa pili, nyumba, shamba na vilevile alimnunulia gari la kutembelea.
Sasa professa alipofariki Dunia 2012. Watoto wake walikuwa bado wanasoma chuo Nje ya Nchi. Yule Mama aliteka mali zote kuanzia viwanja, Nyumba, Magari, Pesa kila kitu kachukua. na ameshafungua kesi Mahakama kuu anataka kibali cha kusimamia Mirathi. Hio kesi bado haijaisha ipo mahakamani mwaka mzima sasa na inaelekea ushindi upo kwa yule mama. (Mke wa pili)
Wale watoto wa marehemu wamerudi Dar hawana chochote hawana mahali pa kukaa, wanakaa kwa ndugu zao. wanapata shida kweli. Yule Mama wa kambo anaendelea kutesa tu na magari ya Professa.
Ndugu wamejaribu kuwapigania kesi hawa watoto lakini wanakwama kwa sababu yule Mama wa kambo kahonga pesa kila sehemu na Ushindi unaelekea kwake. Marehemu Hakuacha wosia kabisa. Naomba ushauri wa kisheria. Hawa Watoto wake wa kwanza watapata haki zao kweli?
 
Duh aisee ndio mana watu wanauana hela hizi mweee! Mie sio lawyer ngoja watakuja
 
Pa zito hapo lakini wenye fani zao wataangalia wapi pa kudadavua ukweli uweke haki kwa wote
Inshu kama hiyo zilitokea na zinaendelea kutokea kwa nchi kama ya kwetu haki inanunuliwa japo si kwa wote
 
Huyo Mama wa Kambo sawa ana haki zake lakini kitendo chake cha kwenda kufungua Mirathi Mwenyewe Mahakamani bila kumshirikisha mtu yeyote halafu anataka Mali zote za Marehemu azimiliki yeye mwenyewe hio ni ishara mbaya na imeshaonyesha kuwa ana tamaa na hajali maslahi ya watoto wa Marehemu.

Nawaonea huruma hao Watoto wa professa maana ni watu wazima halafu wanataabika na maisha huku Mama wa Kambo anaendelea kula kuku kwa Mrija na Magari ya Professa anaendelea kutesa nayo.
 
Nadhani hata hiyo mahakama ina matatizo. Navyojua mimi maamuzi ya usimamizi wa mirathi hupendekezwa na kikao cha wanandugu iweje huyo mama afungue kesi ya kuwa msimamizi bila kushirikisha ndugu?
 
Bwana Maendeleyo. Hii ni Hadithi ya ukweli na watu wanaifahamu vizuri na wapo maprofesa kibao wa Chuo kikuu wanaijua hii hadithi.

Msimamizi wa Mirathi yupo alichaguliwa na ukoo lakini yule Mama wa kambo kapinga kasema ndugu wanataka kumyanganganya mali zake kwahiyo hatambui msimamizi wa mirathi. kwahiyo kaenda mwenyewe mahakamani kufungua kesi ya mirathi mahakama kuu na mpaka sasa hii kesi ipo mahakamani kwa mwaka mzima sasa.
 
Hao watoto nadhani wana umri wa miaka kumi na nane na zaidi kama hawaridhiki na jinsi mama was kambo anavyotaka kuhodhi mali walieleze mahakama tu
 
Huyu mke wa pili si wamachame kweli?

Dah!! Huyo mke wa pili ni mchaga lakini sitaki kusema ni mchaga wa maeneo gani kwasababu ntasababisha watu waanze kutoa maoni mengine ambayo haina maana. cha msingi nahitaji msaada wa ushauri kwa hawa watoto wa Marehemu Profesa kutoka kwenu.
 
Kisheria hana haki na zile mali za wakati profesa akiwa na mzungu na as far as watoto wapo then hatakuwa na ujanja hata tone. Rushwa haitamsaidia kwa hilo.
 
Tatizo ni kwamba haki zinanunuliwa siku hizi. Huyo Mke wa pili mpaka sasa tunavyoongea anashikilia mali zote za marehemu na pesa za kodi ya Nyumba na Pension ya Marehemu zote zinaangia kwenye akaunti yake mwenyewe. Kiufupi ni kwamba yupo kwenye kipindi cha neema. Ndio Maana hata huko Mahakamani Kesi hakijaeleweka mpaka sasa. Sijui wanajamii wa JF Mnashauri vipi kuhusu hii tatizo na hawa watoto wa Professa waanze wapi maana wamekwama kabisa.
 
Back
Top Bottom