Msaada wa kisheria: Nilipigwa na kuvutwa korodani zangu na Mapolisi

Pole sana mzee. Hiyo ikulu imeguswa hata angekuwa JK angeita jeshi zima kwa kupiga ikulu. Komaa walau ujue mustakabali wako. Haki za binadamu bongo wakishindwa kukusaidia nenda Amnesty Int'l kabisa. Hiyo ngoma nyeti sana.
Labda swali moja la msingi ni je tayari ushafanikiwa walau kuzaa watoto kadhaa? isije ikawa jamaa ndo wameharibu kabisa kiwanda cha production ya naniliu ukashindwa kunaniliu bureeeeeeee.
 
Pole sana, kuhusu hilo la polisi nadhani wataalam wa sheria watakusaidia kupata haki yako. Ila hilo la maji na mamlaka ya maji nakushauri peleka malalamiko yako EWURA wana utaratibu wa kushughulikia malalamiko ya huduma hizo unaweza kupata haki yako kwa upande huo ikiwemo kuchukuliwa hatua kwa mtoa huduma huyo. Ingawa hujasema ni wilaya ama mkoa gani tukio hilo lilitokea. Pole sana tutafika tu katika Tanzania huru.
 
Wanasheria bana, wameminya hata hawampi ushauri wowote. Hawa ni wazee wa fee mbele.... hakuna pro bono wala free advice hapa.
 
Pole kwa mkasa uliokufika.

Mimi si mwanasheria lakini hatua ya kwanza unayopaswa kuichukua ni kutafuta Jedwali la Polisi Na. 3 yaani PF3 iwapo ulipelekwa hospitali na ripoti ya daktari ambapo ulitibiwa. Kama hutopata PF3 basi ripoti ya polisi inatosha.

Kutegemea na mkoa ambao unaishi, tafuta tawi la asasi inayotoa msaada wa kisheria, NOLA au nenda kwenye Kituo cha Msaada wa Kisheria na Haki za Kibinadamu, yaani Legal and Human Rights Centre.

Watu wengi hukamatwa na polisi, kwa kuwa hawajui haki zao, hupigwa na kuteswa, kisha hulazimishwa kuandika maelezo ya uongo kabla ya kuachiwa. Nimeshuhudia hili.

Usiogope lakini jiandae kwa changamoto. Andika maelezo yako yote kwa umakini. Taja majina ya wahusika wote. Kama kuna mashahidi ni vizuri uwajumuishe na kuwashirikisha. Shahidi ni mtu ambaye alishuhudia ulivyoteswa, iwe ni kabla, wakati wa, au baada ya. Kwa mfano, kama kuna mtu alikusaidia kukupeleka hospitali, huyo ni shahidi japokuwa hakuwepo wakati unapigwa. Ni shahidi kwa kuwa anajua kwamba ulipigwa na alikupeleka hospitali.

Kila la heri.
 
Zinapiga kazi kaka. Nashukuru Mungu
 
Nashukuru kwa ushauri. Chuo niliendelea badae...na sina kazi kwa sasa.
 
Nashukuru Sana kwa ushauri
 
Nashukuru Mungu kwa watoto wawili now. Kazi napiga kama kawaida. Tatizo ni miguu..nilienda TMJ last month...wakasema mguu mmoja umeachia chini ya kisigino. Napata maumivu makali sana...natumia dawa now
 
Nashukuruni saaaaana wadau kwa comments zenu. Nashukuru kwa maelezo mazuri pia. Ila cha kuongeza ni kwamba...documents zote husika..za ngazi zote ninazo. Na hali yangu kwasasa kutokana na kichapo..sasa ndio naanza kupata maradhi. Mfano..majuzi nilienda TMJ Hospital..nikaambiwa mguu wangu umeachia chini ya unyayo...hapa napata maumivu makali sana na naendelea na matibabu. Nitawampa yatakayoendelea baada ya mwezi mmoja. Nashukuru kwa kunipa picha juu ya swala hili. Tukio lilitokea july 2008 Wikayani Magu..mkoa wa mwanza...polisi kumi na moja walihusika. Majina yao yapo makao makuu kitengo cha malalamiko...na polisi mkoa wa mwanza. Na barua za siri za kujibiwa kutoka ofisi hizo mbili ninazo...hakuna cha maana walichoandika. Nashukuru kwa mawazo yenu.
 
Pole sana kaka ila "kisasi" ni kitu bora sana na kama utasamehe ni bora zaidi,nasema hv kwa7bu kesi kama ya dizain yako ni nying sana na hazishughulikiwi ipasavyo so ukipapa pesa sheria mkononi2!
 
Cha msingi hutopata haki chini ya uongozi huu wa CCM. Je Korodani zinapiga job fresh? au ndio umekuwa mdebwedo?
 
Maisha nilivyofika gerezani hiyo siku ya ijumaa. ..nilikuta wafungwa ndio wanataka kulala hiyo saa 9 au kumi kama sikosei. Nikiwa pale getini..mbele ya wafungwa wote ambao walikua wakiniangalia pale getini...nilivulishwa nguo zote. Nikabaki uchi wa mnyama. Nikachunguliwa matakoni nikiwa hoi nimelazwa chini kwani nilikua siwez kusimama wala kukaa.


Wakati wa kulala...nikalazwa kwenye blanket la sufi chini...tulikua tumebanana sana. Baridi kali...hakuna kujifunika. Nililala na mtu aliyekua kapigwa pia..so vidonda vya mwili wangu na mwili wake viligusana kwasababu ya kubanana.


Maisha ya jela ni magumu sana. Nawashauri wanajf..kama unandugu huko..ni bora ukawa unaenda kumtembelea mara kwa mara na kumtia moyo...Mungu atakubariki sana.
 
Daah alafu utasikia nchi ya amani,katiba imevunjwa hapa
"Vox popoli vox dei"
 

mbona hujaelezea ulichoandika kwenye kichwa cha habari?
 
Aise yaani maji ambayo ni uhai ndiyo yamepelekea mateso yote hayo kwako?. fuata maelezo uliyoshauriwa hapa na uyafanyie kazi, unapokwama usisite kuleta feedback hapa.
 
Nashukuru...nitafanya ivyo.
 

Pole sana kijana, walivyokuvua nguo ilikuwa ktk mazingira gani, hawakukufanya chochote mkuu? Pia ulishacheki afya baada ya kutoka huko maana huwezi jua uzima wa yule mtu mliyegusana mlivyolazwa pa1!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…