Msaada wa Kisheria

Msaada wa Kisheria

Joined
Aug 26, 2018
Posts
13
Reaction score
4
Hivi kuvaa nguo inayotaka kufanana na sare za jeshi kama hiyo kwenye picha ni kosa kisheria?
IMG_20180827_173239_6.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sidhani kama hiyo BUKTA ina-bear definition ya "UNIFORM".

KWA MUJIBU WA KANUNI ZA ADHABU, SURA YA 16, KAMA ILIVYOFANYIWA MAREJEO MWAKA 2002, KIFUNGU NAMBA 178; ni uhalifu kuvaa Uniform ya Jeshi / Polisi kama wewe si askari au mwanajeshi wa majeshi mbalimbali yaliyopo nchini. (jeshi la polisi, jeshi la magereza, Jeshi la JWTZ nk).

Sio tu kuvaa Uniform hiyo, bali pia kuvaa uniform inayofanana fanana, au yenye kutaka kufanana fanana hivi na uniform husika.

Vilevile ni Uhalifu kuvaa mavazi ya jeshi/ Polisi, au mavazi yanayofanana na uniform za jeshi/Polisi, KWA MALENGO YA KUDHIHAKI MAVAZI HAYO.

Adhabu yake ni kifungo CHA MWEZI MMOJA JELA.

LAKINI MTU ATARUHUSIWA KUVAA UNIFORM HIZO ENDAPO ANAFANYA MAIGIZO YA JUKWAA, AU KAMA ANAFANYA STAGE SHOWS ZA MUZIKI, AU KAMA ANAFANYA MAONESHO YA GWARIDE LA JESHI.

Cc Malcom Lumumba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom