Msaada wa kisheria

Ifururu

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2017
Posts
562
Reaction score
658
Habari za asubuhi wana Jamii forum wenzangu.nahitaji msaada wenu maana kuna mambo nahitaji kuyaweka sawa kwa jirani yangu .

Jirani yangu ameachana na mme wake lakini mme hataki kutoa talaka ,yapata mwaka na nusu sasa.Hivyo anaomba kujua kama ataweza kupata talaka kwa amri ya mahakama ili tuu aolewe na mtu mwingine maana ameshampata

Sasa afuate taratibu zipi ili aweze kupata talaka yake kwa kupitia msaada wa sheria.
 
Inatakiwa aanze hatua za mwanzo kabisa kabla hajaenda mahakamani.kama ni mkristo inampasa apitie kanisani walipofunga ndoa,aeleze hali ilivyo.Hapa inatakiwa kuwe na sababu maalum ya kuvunja ndoa hio. Hapa kama mume ndio aliemuacha mke, basi mke anaweza kutumia sababu ya kutekelezwa( desertion, abandonment). Kanisa wakishindwa kusuluhisha watatoa cheti,barua inayoonesha wameshindwa kusuluhisha,na hatua za mahakamani zitafuata.Cha kuzingatia inatakiwa kuwe na sababu kubwa ambayo haifai kurekebishika na ndoa imeharibika kabisa 'irrepeably broken' ndio talaka kuweza kutolewa.
 
Arudi ajenge ndoa yake aache kutanga tanga maisha ya ndoa ni Yale Yale nako huko utaomba taraka
 
Sawa nashukuru,nitaongea nae
 
Hakuna cha jirani hapo ila ni WEWE.

Dini yako ni ipi tafadhali.

Ndani ya mwaka mmoja ndoa imeleta mzozo na tayari ushapata mume?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…