Bubu Msemaovyo
JF-Expert Member
- May 9, 2007
- 4,120
- 3,468
Nina ndugu yangu alikuwa na kesi alishitakiwa kwa wizi wa matunda toka shambani. Aliyemshtaki ni mvamizi katika shamba hilo. Huyu ndugu yangu alikuwa anachunga matunda yake. Mvamizi huyu wa shamba ambaye anadai shamba na matunda ni vyake alienda mahakamani. Kesi imeendeshwa na kumpa ushindi huyu ndugu yangu. Akaachiwa huru baada ya hakimu kusema "Ushahidi ni wakujichanganya sana".
Mshitaki akakata rufaa. Akidai hajaridhishwa na uamuzi wa Mahakama. Anasema Mahakama haikuzingatia evidence alizozitoa hivyo anaiomba Mahakama ya Wilaya ipitie upya mwenendo mzima wa kesi.
Swali langu:
Huyu ndugu yangu ambaye mahakama ilimuona hana hatia hii karatasi ya rufaa anatakiwa afanyiwe nini kisheria? Je, kuna jambo anatakiwa kujiandaa siku ya kufika mahakamani?
Swali limekuja baada ya Hakimu kumwambia ndugu yangu aandae majibu ya kumjibu aliyekata rufaa. Je, ni sahihi? Kama hana imani na Mahakama ya Mwanzo mshitakiwa ajibu nini katika rufaa hii?
Mshitaki akakata rufaa. Akidai hajaridhishwa na uamuzi wa Mahakama. Anasema Mahakama haikuzingatia evidence alizozitoa hivyo anaiomba Mahakama ya Wilaya ipitie upya mwenendo mzima wa kesi.
Swali langu:
Huyu ndugu yangu ambaye mahakama ilimuona hana hatia hii karatasi ya rufaa anatakiwa afanyiwe nini kisheria? Je, kuna jambo anatakiwa kujiandaa siku ya kufika mahakamani?
Swali limekuja baada ya Hakimu kumwambia ndugu yangu aandae majibu ya kumjibu aliyekata rufaa. Je, ni sahihi? Kama hana imani na Mahakama ya Mwanzo mshitakiwa ajibu nini katika rufaa hii?