Msaada wa kisheria

Msaada wa kisheria

irumba1

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2013
Posts
882
Reaction score
321
Nilikuwa na mchumba wangu ambaye nilitaraji kufunga ndoa nae ya kiislam,maandaliz ya harusi yaliendelea vizur sana na nilifanikiwa kujitambulisha kwao na pia kulipia mahari kwa asilimia 85,lakin baada ya kulipia mahar wazazi wake wakawa wananilazimisha nifanye haraka hiyo harusi lakini kutokana na mimi kuwa mbali kikazi niliwaomba wanivumilie.hata hivyo baada ya miezi kama 6 toka nilipolipa mahari wale wazazi wakaruhusu binti yao akaolewa na mtu mwingine,Sasa wana jf haki yangu ni ipi katika hili?,nidai mke au nidai mahari?,sheria za kiislam zinasemaje? Na je sheria zetu kwa ujumla zinasemaje kuhusu hili?.msaada please
 
hapo ndugu unatakiwa kudai mahari na garama zote ulizozitumia kwake kwa ushahidi; mfano ,ulimnunulia vitu ukavipeleka kwa kupitia washenga, gharama ulizotumia kwenye sherehe ya ulipaji mahari na garama yeyote ile. uende kafungue kesi ya madai mahakamani. nitakuattachia sheria ya Ndoa tz hapa, lakini kwa sasa kabla haujasoma hiyo sheria nitakayoweka kwa pdf hapa, bofya hapa SHERIA KWA KISWAHILI utapata kitabu cha sheria kwa kiswahili ambamo ndani yake kuna sheria ya ndoa, hata hayo mambo ya kusalitiana uchumba yamewekwa na vifungu vya sheria vipo.

kwenye sheria hii nitakayoattach, soma kifungu cha 69,70 na 71.
View attachment 103895

ukishasoma hiyo sheria, nakuwekea hiyo link uende kule utapata kitabu hiki hapa chini SHERIA KWA KISWAHILI

View attachment 103896View attachment 103896View attachment 103896
 
Back
Top Bottom