NAMTUMBA
JF-Expert Member
- Feb 20, 2014
- 1,939
- 597
Naomba msaada wa kitaalamu. Mm ni Mkulima wa Korosho huku Mtwara. Nimeuza shamba langu la Korosho kwa milioni moja na nusu (1,500,000) lengo langu ni kujenga kiwanda cha kubangua korosho ili kuunga mkono juhudi za awamu hii. Nimeona niuze shamba langu nipate mtaji wa kufungua kiwanda maana nimevutiwa sana na kasi hii. Nasikia nikiwa na laki tano naweza kuagiza kiwanda kizuri tu na chakisasa. Nisaidieni utaratibu namna ya kupata Kiwanda na jinsi ya kupata kiongozi mkubwa aje kuzindua na kukata utepe.