Hebu mtoa mada nieleweshe jambo moja: Kwa uelewa wangu wa kifamasia na kemia,zipo siku tano(5) ambazo mwanamke uki... anaweza kupata mimba. Siku nyingine zooote ni zako mnafanya mnachotaka(isipokuwa siku za menstruation) .
Sasa swali langu ni kuwa, ulishindwa kabisa kuvumilia hivo visiku ukaponzwa na matangazo NYOTA YA KIJANI ukachoma sindano... Haya basi,baada ya kumchoma sindando mlikuwa mnafanya kila siku na kila mara?
Mimi ni mfamasia,na mke wangu siwezi mruhusu afanye hivo maana sisi wafamasia tunafahamu athari zake...kama kuongezeka uzito,presha insulin resistance na baadae kisukari.
Tatizo tunawafanya wanawake vyombo vya starehe, wanatufia tunabaki kulea watoto wenyewe.
Nnachokushauri wewe na wengine ni kutumia condom na njia nyingine zisizohisu kuingilia mifumo ya hormone ya mkeo.
Si salama hata kidogo kma inavopigiwa debe na vyombo vya habari.
Kama kweli unampenda,utamlinda.
Mwenye macho na aone na mwenye masikio asikie.