Msaada wa mawazo wasomi

GITWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
1,572
Reaction score
1,781
Ndugu yangu ana umri wa miaka 40, ameniomba ushauri wa kusoma, anataka kufanya mtihani wa six kama PC ili aende chuo kikuu. Kwa sasa yeye ni mjasiriamali na credit zake za O level ni hkl. Swali linalomsumbua ni kuwa je hiyo elimu anayotaka kuiendea itamsaidia? Au ang'ang,ane na biashara zake tu. Na iwapo atasoma na kufanikiwa kwenda chuo kikuu je achukue taaluma gani?

Hayo maswali yameniwia magumu nikaona nilete kwa great thinker mnisaidie. Nakaribisha mawazo mbalimbali lakini sio kejeri.
 
Biashara wanachukua watu wa hkl
 
Je? Biashara wanachukua watu wa hkl.

inawezekana mtu wa hkl akasoma biashara almradi tu amudu hesabu za biashara. mi nafikiri biashara ni discipline ambayo mtu yeyote anaweza akasoma. kitu ambacho hufanyika ni ushauri tu kwa mtu ambaye hakusoma hesabu kwa kuhofia kuwa anaweza asimudu hesabu za biashara. vingenevyo mi naona asome biashara.
 
Asante mkuu nitajaribu kumshauri
 
Business administation iko poa kwake anaweza soma huku anafanya yake aende vyuo kama IFM TIA CBE etc wanapokea na itakuwa vizur kwake sababu inauhusiano na anachofanya kuna dada yangu nae anafanya hvo
 
Ye yupo morogoro. Je Moro hakuna chuo anachoweza soma. Ili iwe rahisi kwake kuwa anatokea nyumbani
 
Ye yupo morogoro. Je Moro hakuna chuo anachoweza soma. Ili iwe rahisi kwake kuwa anatokea nyumbani

kutoka moro had dar n cheap kama sh 5000 hv so anaweza kukaa moro akawa anasoma dar kila siku bila shida
 

Huyo ni mtu mzima sana, kuanza kusoma A level. kama ana lengo la kusoma biashara, namshauri akasome Diploma kwanza ya Biashara ambazo vyuo vingi vina options za jioni. Akimaliza hapo atakuwa na equivalent qualifications to bachelor. Kusoma DIPLOMA kutampa ABC za Degree yake na kwa hiyo akiingia hata Business bado ataimudu vizuri. Kusoma A level kutampotezea muda as tuchukulie Principals zisipopatikana once. Atazeeka huyo mzee mwenzangu. Lakini pili ajue kusoma ni maamuzi kwanza lakini pia kusoma ni malengo. Kama anadhani kusoma kutamfanya asogee mahali fulani kibiashara ni vizuri namshauri apambane mpaka mwisho, but siku hizi tunazoziendea huko Mbele Elimu ni kibao tu ambacho unabaki umekivaa na hakikufikishi popote. Kwake yeye akisoma amaanishe elimu imsaidie kuboresha anavyovifikiria na kwa upande mwingine elimu itapanua upeo wake na kwa hiyo atakuwa anaona avenue nyingi kuliko asiye na elimu. Mr. Sisera.
 
Morogoro kuna muslim university of morogoro kuna mzumbe university pia kuna jordan university collage ajaribu kuvicheki hivo
 
Ye yupo morogoro. Je Moro hakuna chuo anachoweza soma. Ili iwe rahisi kwake kuwa anatokea nyumbani



Kwa Morogoro,aende JORDAN UNIVERSITY,kipo maeneo ya Nanenane na wanatoa course ya BBA(Bachelor of Bussiness Adminstration).
Pia kuna watu wamesoma HKL&HGK A-Level na wanasomea course hiyo hapo,kwa sharti tu uwe umefaulu Math O-Level.
 
Wakuu nashukuru sana kwa michango yenu na ninaendelea kuipokea na kujadiliana nae.
 
Akasome Small bussines and entrepreneurship au BBA na kama formsix akifanya pepa akichemka basi akasome tu ngazi ya cheti then dip then degree
 
Ye yupo morogoro. Je Moro hakuna chuo anachoweza soma. Ili iwe rahisi kwake kuwa anatokea nyumbani
kuna jordan university mbona.na vingine vingi tu.asiogope.ubaya ni mda sasa maana atakuwa busy na biashara na kusoma kidogo,kama anasoma basi aweke mtu awe anamsaidia usimamizi alafu ndio afanye masomo kiufanisi fasta atakuwa chuo kikuu na atafulfil dreams....namshauri asome BACHELOR OF BUSINESS ADMINISTRATION MAJOR IN MARKETING),haya pia kama alipata angalau D hesabu anaweza soma hata IFM ,cbe, kwa mambo ya biashara.
 
Shukrani. Nafurahi kuona great thinkers mlivyo na michango mizuri.
 
Jamaa Ana credit ngapi jumla? Kama ni tano anasifa ya kujiunga na diploma, na Kama Ana tatu anasifa ya kujuunga na cheti. Asisome six inahitaji muda mwingi sana.
 
Jamaa Ana credit ngapi jumla? Kama ni tano anasifa ya kujiunga na diploma, na Kama Ana tatu anasifa ya kujuunga na cheti. Asisome six inahitaji muda mwingi sana.

Ana C tatu na D mbili zote masomo ya art anaweza chukua cheti gani?

History C. Kiswahili C. English C. Bible D. Civics D.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…