Biashara ya mazao hasa nafaka faida zake kwa unit ni ndogo sana.
Kwa sababu hiyo unatakiwa kukuza faida (maximize profit) kwa kuuza kiasi kingi cha mazao (high volume).
Hii ina maana kuwa unatakiwa kuwa na mtaji mkubwa.
Shilingi 3m hazitoshi kukuletea faida ya haraka kwa kuyasafirisha mazao toka sehemu moja kwenda ingine.
Kwa kiasi cha chini sana cha kuanzia unatakiwa uwe na uwezo wa kununua mazao ya kutosha kujaza lori la tani 30.
Kwa mfano kama unanunua mahindi mikoa ya Kusini kwa bei ya shilingi 600 kwa kili, unatakiwa kuwa na shilingi 18,000,000 kuweza kujaza lori. Gharama zingine pia ni kama vifungashio, kupakia, kushusha, usafiri, ushuru na gharama zako mwenyewe.
Kitu muhimu sana cha kuzingatia wakati wa kununua mazao ni ubora wake.
Ubora wa nafaka yoyote unazingatia vitu vifuatavyo.
1. Moisture content ( nafaka nyingi haitakiwi kuzidi 13%)
2. Colour grade
3. Free from mould
4. Free from foreign matter
5. Standard grain size
6. No odor smell
etc
Pia kitu kingine cha kuzingatia ni kujua bei ya soko unakota kwenda kuuza mazao yake na ufanye mchanganuo ( costing) ili ujue ni kiasi gani cha faida utapata kwa kwenda kuuza mazao yako.
Hii biashara ya mazao ina hatari nyingi (high risks) za kupoteza pesa zako zote kutokana na vitu vifuatavyo.
1. Kuharibika kwa mazao wakati yanasafirishiwa, kwa mfano kunyeshewa mvua au kuingia maji.
2. Mazao kulowana kwa mafuta kama diesel au mafuta ya taa
3. Kuanguka kwa Bei.
4. Wizi.
5. Kutapeliwa na madalali
6. Mazao kuharibika kwenye ajali ya lori lililobeba mazao.
etc
Nakushauri usijiingize kwenye biashara ya mazao kama huna uwezo wa kutatua changamoto zilizotajwa hapo juu.
Ungana na mtu mwaminifu na mwenye uelewa wa biashara hii ili akufundishe na kukuelimishe kabla hujabaki mwenyewe.