Nisaidieni wakuu, nina mgeni toka China alikuwa na kibali cha tourist cha miezi 3, Bado hakijaisha but amebakisha kama siku kumi, nataka aendelee kuwepo yaani aongeze mda wa kukaa mwenye kujua process zake nisaidieni kabla mda wake haijaisha.
natanguliza shukrani zangu!
tourist visa maana yake alikuja kutalii au kutembelea ndugu zake . na hiyo visa inalipiwa dola 50 tu. na inakuwa ni ya siku 90 au miezi 3. kwa kawaida hiyo visa ikiisha huwa haiongezwi kabisa hata iweje . na asije mtu akakudanganya atakulia hela yenu bure. kwa kukusaidia mwambie apande basi au ndege atoke nje ya tanzania let say aende kenya,zambia au nchi yeyote jirani na tanzania akae hata siku moja au mbili then ageuze arudi tena tanzania atapewa tena hiyo tourist visa ya miezi mitatu. kwa kuepusha gharama zaidi mwambie aende nairobi na kurudi kupitia border ya namanga arusha
Mkuu nashukuru kwa msaada wako mkuu!
Ngoja nifanye hivyo tuu!
Zaidi ya miezi mitatu sio kutalii tena bali ni kuhamia ndugu,huyo ni mhamiaji,maake hata kiswahili keshajua hata kukiongeakwanini unasema si mtalii mkuu!?