Msaada: Wanauchumi nitawezaje kusave mshahara wa laki moja na ishirini, ili nami niwe na mafanikio?

Uangalie usipate vidonda vya tumbo..hiyo hela tumbua yote na utafute nyingine ule.. ukipata zaidi ya 300k ndio atleast unaweza kucheck possibilities za kusave.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Weka sura yako humu kk/dd
Mjini hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pia kumbuka shida ya mentality ya kusave ni kuweka fedha kwa matumizi ya baadae, deferred expenditure hii haina maana, unajiandaa kuweka kwenye matumizi baadae. Ingekuwa vema, ukiweka kwenye kuwekeza hiyo elfu thelathini unayoweka ikakuletea hata elfu tatu kwa mwezi ukiokaa, kama hiyo hela unayoweka inazalisha ni sahihi, ila kama imepaki tu haileti wenzake mpango huo haufai. Tafutia kazi hiyo hela utakayoweka ili ilete hela nyingine. Hakikisha kazi utakayoipa hiyo hela unaijua vizuri na sio kitu cha bahati nasibu, bahati nasibu sio kazi ya kuipa hela yako uliyojijima.
 
Mkuu mbona wewe una muda wa kutosha kabisa wa kupata pesa nyingi Sana Kama kazini unatoka saa 10 ni muda mzuri Sana Mimi naenda kazini saa 1 kutoka saa 12 jioni naishi igoma
Ni bora ata kazini ningekuwa natoka saa 12 kamili uwa natoka na dk 45 au siku nyingine saa moja na dk 6 kwenda kupanda gari paka kufika igoma nafika saa 2 nikifika igoma Kuna kibanda changu nauza sigara maji juisi na vindala nafungua nauza kwanzia saa 2 paka saa 5 usiku naenda kulala uwa siku azilingani ipo siku hali mbaya ipo siku hali nzuri inategemea ila kwa huo muda tu uwa napata faida sikosi kwa kiasi chake kwasababu ipo siku nitapata faida elfu 10 ipo siku napata elfu 2 siku nyingine faida elfu 20 uwa ninaweka malengo kila ikifika jumapili uwa kwenye faida yote ya wiki natoa elfu 14 naweka akiba nyingine nazungushia biashara na maitaji madogo mengine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hongera kwa uamuzi wa kuanza kusave swala la kuweka akiba ni tabia au culture ambayo ni natural blessed au mtu unaweza kujifunza na kujizoesha..Kama hauna utamaduni wa kuweka akiba ata upate million 5 kwa mwezi Ni ngumu kuweka akiba...Kingine ni lazima kuwe na strong purpose ya kufanya saving bila hiyo utakosa passion ya kusave na utachoka. Fanya utafiti ni biashara gani ya mtaji wa laki tano unayoweza kufanya ukitoka kazini tumia opportunity ya kuwa lake zone biashara zinafanyika holela..laki tano inatosha kupata robota zuri la mashati ya kiume weka kwenye racket ukitoka kazini Mwaga mzigo ata nje ya Bank hakuna shidda.. muhimu kitambulisho Cha machinga saa 10 mpaka saa 12 utakosa wateja.. huo mshahara wako ni mkubwa Sana unaweza save nusu yake tsh-60.. sacrifice for your future..
 
Kama kweli unalipwa Tsh 120,000/= kwa mwezi

Toka chumba cha Tsh 30,000/= nenda chumba cha Tsh 10,000/= au 15,000/= kwa mwezi

Nenda kaishi karibu na kibarua chako kilipo, ili uachane na kulipa nauli

Tafakari kama kazi yenye malipo ya Tsh 120,000/= itakufanya utimize malengo yako

Unaweza ku save Tsh 50,000/= kwa mwezi kuanzia mwakani

Goodluck
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jitahid kusave ata 10k kila mwezi baada ya miez mi5 inaweza ikawa ni 50k. baadae unaweza kupata chochote unachoweza kufanya kwa hio 50k ikakupa ata 1k kwa SKU.
Nihesabau Mbovu lakin inaweza kukuimarisha kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nina imani una smart phone

Ukipata mshahara toa 30,000/=
Agiza hereni 10*3000=30,000/=
Post kwa status yako au nenda nazo kazini kwako
Uza hereni moja 5000 au 4000
4000*10=40000/=
5000*10=50000/=

hakikisha hiyo elfu30 unaizungusha kwa huo mwezi mzima ili mshahara ukukute

tuashumu umezungusha Mara 5
10,000*5=50000/=
20000*5=100,000/=
Fanya hivyo mpaka mtaji ukue
 
Mdau nimeona una wazo zuri lkn kwa mshara huo ni ngumu sana kusave. Ila nikushauri kitu kimoja kama hutojali lkn, hapo mwanza kuna ziwa naomba uachane na hicho kibarua ukatembeze dagaa wabichi. Kama kweli una moyo wa kujiajiri utaleta mrejesho wako baada ya miezi kadhaa. Mie nakwambia hayo kwasababu baada ya kumaliza form 4 nilianza kusaka kazi ktk viwanda vya samaki pale ilemela pasipo mafanikio! Lakini nikapata wazo la kutembeza dagaa wabichi kwa baiskeli za kukodi sikujuta hata siku moja. ila badae niliachaga kwa sababu ya kuendelea na masomo. But kwa msaada zaidi namna ya kufanya biashara na kusave nichek pm
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…