Tatizo la Jf ni wakati mwingine unakuta mtu ana shida au tatizo then wengine wanaleta jokes, mkuu mm yamenifika na anachosahau huyo ndg hapo juu ni kuwa situation km hii inaweza kumkumba yeyote yule, hivyo km tukipeana elimu hapa, likitokea la kutokea hapa wako watakaoweza kujifunza.Unamshutumu mwenzio wakati avatar yako ina picha ya Rais, kwamba ndiye aliyeandika hayo maneno machafu. Hivi ukikamatwa utasema umeonewa au kuwa yeye ndiye amekuruhusu kutumia picha yake na hayo maneno?
Unatuponza tunaotumia jf kupashana habari na kuelimishana.
Unampotosha ajichukulie sheria mkononi atafungwa. Aende akatoe taarifa polisi.Hiviii kwelii unataka kutwambia umekosa cha kumfanya kabisa kabisaa mpakaa ufedheheke namna hiii? Mtu alishakuwa kituako jinsi yakumpata sidhan kama inakushinda nahis na Picha ulimtumia mwenyewe nakama anakupost sema anaandika caption za mahaba we unadata sababu umeoa na MKE na ndugu wamesanuka sasaa Kama hujuii taratibu zakufuataa. Tafuta zake nawewe post uandike madudu yako
Sent from my Infinix NOTE 3 using JamiiForums mobile app
Mkeo kama ni mwelewa na anakutunza vema kama mumewe ataweza kutambua picha zakabla na baada ya nyie kuoana hivyo hawezi kukuletea shida.Kwa kifupi kuna dada nilishawahi kuwa na mahusiano nae kipindi cha nyuma kabla sijaoa, baadae nilioa tena kwa ndoa takatifu kanisani, katika siku za karibuni amekuwa akipost picha zangu katika mitandao mbalimbali ya kijamii na kuandika maneno mbalimbali ya kidhalilishaji yanayoniletea shida sana kwenye ndoa yangu, kwenye familia yangu kiujumla kwa maana ndugu zangu wamekuwa wakisumbuliwa sana na hii hali, naombeni msaada wenu nifanyeje, sheria inasemaje.