Msaada wenu Wakuu, baba yangu hataki kunilipa deni langu

Msaada wenu Wakuu, baba yangu hataki kunilipa deni langu

Wewe jamaa wa maajabu sana kwenye hii dunia, unaanzaje kumdai mzee?

Mwanzo nilijua ni kitoto cha miaka 12 kimekuja kutovuka adabu hapa, kumbe ni wewe umejaza nywele kila chochoro ya mwili wako! (inasikitisha sana)


Miaka 32 upo nyumbani bado, hivi hiyo akili yako ipo sawa kweli?


Je ukiambiwa huna adabu utapinga?


Kwakweli mzee wako hajivunii/anasikitika kukupata kijana wewe
(hivi unaroho ya chuma ama vipi? )



UNAMKOSEA SANA MZEE WAKO HADI AIBU NAONA MIMI


BADILIKA KIJANA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habarini za uzima wakuu

Mimi ni kijana nina miaka 31, mwaka huu mwezi wa pili mungu akipenda natimiza 32 (kwa kweli litakuwa jambo la kumshukuru Mungu kwa uhai huo)

Niende kwenye maada moja kwa moja

Kipindi nipo chuo 2013 nilikuwa napata bumu langu vizuri tu, baba yangu aliniomba nimsaidie sh laki 5 kipindi nipo mwaka wa pili nikampa kwa miadi kuwa atanirejeshea pesa yangu.

Mwaka wa tatu semister ya pili mzee akaniomba laki 4 tena uku akiwa bado hajanilipa laki 5 yangu, sikuwa na iyana nikampa

Jumla nikawa namdai SH LAKI 9 (900,000)

Baada ya kumaliza chuo na kurudi home ni mwaka wa 7 sasa baba hataki kunilipa deni langu

Umri wa kuondoka nyumbani umeshakaribia, nimemuomba mzee anipatie iyo pesa yangu nikapange chumba nifungue na biashara ila kila siku anasema hayupo vizuri

Wakuu naombeni ushauri wenu nifanyeje nipate haki yangu

Maana nikimuambia mambo ya siasa anasema kama naipenda CCM niondoke nyumbani kwakwe, wakati huohuo hataki kunipa ela yangu

Kila siku is naumia moyoni

Naombeni msaada wenu

Sent using komputa mpakato
Achana kabisa na hilo deni, miaka 7 uliyoishi kwa baba yako baada ya kumaliza CHUO wewe ndiye unadaiwa , siku ukiondoka hakikisha unamuachia not less than 1m
 
Achana kabisa na hilo deni, miaka 7 uliyoishi kwa baba yako baada ya kumaliza CHUO wewe ndiye unadaiwa , siku ukiondoka hakikisha unamuachia not less than 1m

Acha kupotosha, chakula kingi kwa baba.... mtoto hurithi kwa wazazi wake na si kinyume chake.
 
Ukiwa hauna pesa unaweza kuona hiyo 900,000 ni kubwa sana so unaweza kuidai kwa nguvu. Ila sasa ukipewa ukaenda kuanza maisha utajikuta hauna kitu. So samehe hiyo pesa. Maana kiutaratibu ulipofikisha miaka 18 tayari ulishakuwa mtu mzima ulitakiwa uishi kwako. Vp mshua akikupigia mahesabu,utatoboa kweli ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu umeongea point sanaaaa....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naamini miaka 31+ ni umri wa mtu aliye komaa kiakili na fikra.

Naamini mzazi wako hakukukopa hizo hela ili akafanyie mambo ya anasa bali ni kwajili ya kutatua jambo linalohusu mstakabari wa familia.
Wewe binafsi pengine kwa namna yoyote ile umenufaika na jambo hilo ukiwa kama mwanafamilia.

Hata kama hiyo hela ni ya Heslb ambayo itakulazimu kulipa, fanya uisamehe tu kwakuwa kaitumia mzazi wako maana hata yeye ingekuwa mmeingia terms za kukopeshana tangu chekechea hadi chuo sidhani kama ingekuwa 900k tu.

Mdogo wangu huko ni kukosa maarifa, acha kubweteka hapo nyumbani na usipokuwa makini utaanza kudai na kumsurutisha mzee akupe urithi wako hata kama leo atakulipa hiyo 900k.

Ondoka hapo chalii kakomae hata maporini huko uchome mkaa upate mtaji kuliko kun'gan'gania pesa ambayo hata kama mzee atatoa, itakuwa haina baraka na haifai kuifanya startup capital.

Kikubwa kuwa na nidhamu ya hela tu na mtaji si lazima uanze na mamilioni.
Hii miaka mitano hapa kati kubali kuchakaa utatoboa.
 
Kwahyo mwanangu umeamua kunianika humu??

Naomba unilipe gharama zote nilizo tumia kukulea.. mbaka ada nilizo lipa huko shuleni


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Habarini za uzima wakuu

Mimi ni kijana nina miaka 31, mwaka huu mwezi wa pili mungu akipenda natimiza 32 (kwa kweli litakuwa jambo la kumshukuru Mungu kwa uhai huo)

Niende kwenye maada moja kwa moja

Kipindi nipo chuo 2013 nilikuwa napata bumu langu vizuri tu, baba yangu aliniomba nimsaidie sh laki 5 kipindi nipo mwaka wa pili nikampa kwa miadi kuwa atanirejeshea pesa yangu.

Mwaka wa tatu semister ya pili mzee akaniomba laki 4 tena uku akiwa bado hajanilipa laki 5 yangu, sikuwa na iyana nikampa

Jumla nikawa namdai SH LAKI 9 (900,000)

Baada ya kumaliza chuo na kurudi home ni mwaka wa 7 sasa baba hataki kunilipa deni langu

Umri wa kuondoka nyumbani umeshakaribia, nimemuomba mzee anipatie iyo pesa yangu nikapange chumba nifungue na biashara ila kila siku anasema hayupo vizuri

Wakuu naombeni ushauri wenu nifanyeje nipate haki yangu

Maana nikimuambia mambo ya siasa anasema kama naipenda CCM niondoke nyumbani kwakwe, wakati huohuo hataki kunipa ela yangu

Kila siku is naumia moyoni

Naombeni msaada wenu

Sent using komputa mpakato
mimi naweza hata kuwashangaa hata wanaopoteza muda kumshauri huyu dogo jibu analo mwenyewe kuwa mzazi hadaiwi hebu msipoteze muda wenu jadirini ya maana
 
Acha kupotosha, chakula kingi kwa baba.... mtoto hurithi kwa wazazi wake na si kinyume chake.
endelea kusubiri chakula na urithi kutoka kwa baba, miaka 32 bado unasubiri laki tisa ambazo ndani ya nafsi yako unajua mzee hawezi kurejesha . amka baba pambana Maisha ni mapambano
 
endelea kusubiri chakula na urithi kutoka kwa baba, miaka 32 bado unasubiri laki tisa ambazo ndani ya nafsi yako unajua mzee hawezi kurejesha . amka baba pambana Maisha ni mapambano

Kwani unateseka, mtoto kwa baba hakui.
 
Miaka 31 bado uko kwa baba na mama....!!?
Huna aibu hata kidogo unaleta Uzi wa kindezi namna hii na chuo umeenda...!!?

Kwa jinsi ulivyo na akili yako mbovu huwezi 1. Kuwajengea wazazi wako nyumba bora hata ukipata mafanikio namna gani.
2. ................. .........
3.
4.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ni MWENDAWAZIMU?
Unapokopa pesa kwa mtu sharti ulipe mara moja kulingana na makubaliano.
 
Back
Top Bottom