Msaada

Mutta

Senior Member
Joined
Mar 24, 2011
Posts
101
Reaction score
11
Rafiki yangu amekuja kuniomba ushauri mgumu,nikaamua niwashirikishe.Yeye ameoa ana miaka 6 kwenye ndoa ya kanisani.Hawana mtoto mpaka leo.Wameenda kupima yeye ni mzima ila mkewe ana matatizo{sijui kama ni ya kudumu au la}.Anataka kutoka nje ya ndoa ili apate mto to maana amejenga nyumba.Wote wana kazi ila mwanaume anachekwa kuwa labda jogoo hawiki.Je nimsaidieje au Ungekuwa wewe una tatizo kama hilo ungefanyaje?
 
Wakae chini wote watafute ufumbuzi, Kama wote nia yao moja mwwnyezimungu atawajaalia,kwenda njee ya ndoa sio jawabu zuri endapo mkewe akijua na hakuomba kua hivyo sass asimsugue roho mwenzake...
 
Kwanza miaka sita, sio mingi sana kwa hesabu za sikuhizi. Labda tatizo umri ukiwa umesogea kujaribu kunaweza kuwabana kidogo. Pili, hilo ni swala gumu sana, tena kujadili kwa kusikia upande mmoja tu! Unahakika mkewe anahitaji mtoto pia? Tatu, mwenzio anapaswa kukuambia wazi nini maana ya mtoto. Ni yule wa damu yake tu ama yoyote watakae lea?
 
1..kujenga nyumba si kiegezo kwamba anapaswa kuwa na mtoto/watoto

2.... ndoa siku zote haihusiani na watoto yale ni matunda ya ndoa na ndio maana kanisani huwa wanasema ..je mko tayari kuwalea na kuwatunza watoto MTAKAOWAPATA?....kumbe mnaweza kuwakosa pia

3...kutoka nje ya ndoa ni kuongeza matatizo

4..akae chini na mkewe waongee na kama mke akikubali hoja ya mzee sawa ....

5....waende vituo vya kulelea watoto yatima waadopt mtoto/watoto
 
Inaoneka umri wa mwanaume umesogea kwenye 40 hivi na mke 30 .Sasa yeye anaona umri umeenda kila akijaribu anabaki ola. Je mke atakubali mwamme atoke nje.Je mali walizonazo {nyumba,gari} atarithi nani
 
Inaoneka umri wa mwanaume umesogea kwenye 40 hivi na mke 30 .Sasa yeye anaona umri umeenda kila akijaribu anabaki ola. Je mke atakubali mwamme atoke nje.Je mali walizonazo {nyumba,gari} atarithi nani

Mwanamke akishaelewa kwamba ana tatizo na nila kudumu, anaweza kukubali.... hadi huyo mama ajue/akubali hilo,mumewe hastahili kwenda kutafuta mtoto nje ya ndoa....watu wanakaa miaka mingi sana....maombi maombi!!
 
Inaoneka umri wa mwanaume umesogea kwenye 40 hivi na mke 30 .Sasa yeye anaona umri umeenda kila akijaribu anabaki ola. Je mke atakubali mwamme atoke nje.Je mali walizonazo {nyumba,gari} atarithi nani
Umri kitu gani bwanaaa. Aachane na mambo hayo. Akae na mke wake kwenda nje sio kigezo cha kupata mtoto.
Kama wamefunga ndoa kanisani waliapa wakasema watavumiliana kwenye shida na raha.
Kumbuka Ibrahim alipata mtoto akiwa na umri mkubwa sana.

Mwambie amgoje Bwana natafanya yeye aache njia za mkato, atapata matatizo badala ya kusolve
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…