Pre GE2025 Msajili apiga Marufuku Kongamano la CHADEMA mkoani Mbeya, asema matamko yao yanahusisha vitendo vya uvunjifu wa amani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Msajili wa vyama vya Siasa amepiga Marufuku Kongamano la Chadema mkoani Mbeya lililokuwa kifanyike kesho Jumatatu.

Msajili amesema matamko ya Chadema yanaashiria uvunjifu wa Amani. Amesema kwa mfano Bavicha wanasema " Siku hiyo tutaweka hatma ya nchi yetu Tanzania kama ambavyo Vijana wa Kenya Gen Z wamejitambua tunaenda kuweka Maazimio makubwa ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi mkuu wa 2025".

Kwahiyo Ili kulinda Usalama wa Raia na Mali zao Msajili wa Vyama vya Siasa amefutilia mbali Kongamano hilo.

Pia soma=> Jeshi la Polisi lapiga marufuku mkutano wa BAVICHA siku ya vijana duniani


 
Ni aibu kubwa sana kwanini asifute upinzani tubaki na sisiemu tubanane humohumo chama kimoja. ? Mnajinasibu kufanya makubwa halafu how come mnaogopa hawa CDM kulikoni?
 
Ni aibu kubwa sana kwanini asifute upinzani tubaki na sisiemu tubanane humohumo chama kimoja. ? Mnajinasibu kufanya makubwa halafu how come mnaogopa hawa CDM kulikoni?
Amani ni muhimu
 
Hapa sasa ndiyo serikali imeshikwa mahali pabaya. Ukiona wapinzani wanafanya jambo na serikali iko kimya basi ujue halina nguvu za kuleta mabadiliko.
 
Kwamba kule Zanzibar vifanyike na state resource halafu kwingine Kuna uvunjifu wa amani. Toka lini ofisi ya kusajilia ikawa na intelligence department? Na kama umepata hizo inteligia mbona hujawashika hao watu wanaopanga hivo vitendo? Maana kupanga tu njama ni criminal offence under the penal code au mmesahau?
 
Msitufokee,mlikuwa mnasema mbaya wenu alikuwa Magufuli, baada ya kifo cheke mlifanya sherehe kuwa mnakwenda kula kuku kwa mrija dhalimu hayupo tena, Sasahivi haya mnayatoa wapi, maana Mama yenu kipenzi na Serikali yake hawana shida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…