Msajili wa Hazina: Serikali kuyafuta Mashirika na Taasisi 40 za Umma zinazozalisha hasara na kutegemea ruzuku ya Serikali kuu

Wahamishwe mazima ,kwani sehemu ya kuishi ni huko hifadhini tuu?
 
Ccm ndio balaa kubwa ktk taifa hili. Utashangaa pale ambapo tumeshawekeza mabilioni au matrilioni watagawa kwa bei ya kutupa. Ni kweli mashirika haya yanatia hassra, lakini tutakapo yauza/kubinafsisha tupate thamani halisi, sio kugawia makada na wafadhili wa ccm. Na nawashanga, kwa mfano Atcl tunajua inatia hasara lakini bado tunaendelea kuagiza ndege za nini?
 
Wanao yaua ni wao na watafanya njama wayafute yale yalionona ili wayanunue wao akina Abduli.
 
Hauko serious,Kawe hawakusahau Bali Mwendazake alichujuaga pesa zao na pia aliwapiga stop kwenye biashara ya nyumba.

Ila Kwa Sasa hapo Kawe mambo Iko hivi 👇👇

View: https://www.instagram.com/p/C_I9NWANH8h/?igsh=Z3V2Mjc5NjBnM29w
Magufuli aliamini hayo majengo ya Kawe ni mradi wa Kikwete hivyo alizuia yasiendelezwe akiamini anamkomoa Mkwere. Hata suala la bandari ya Bagamoyo alilishwa matango pori na ikawa rahisi kwake kuamini kwani mawazo yake yalikuwa tayari ni kuukata uwekezaji ule.

Alikuja kugundua kuwa kaingizwa chaka na akamtimua Mkurugenzi wa TISS Kipilimba.
 
🚮🚮🚮
Hasara ya ATCL inakwenda ikipungua kila mwaka kuanzia mwaka ule lilipoanzishwa upya.

Ndani ya miaka michache sana ijayo hasara hiyo itakuwa imekwisha. Masoko ya bidhaa zenye kuhitaji kusafirishwa kwa ndege yanazidi kupatikana.

Wanatakiwa kuwa makini kwenye upangaji wa ratiba zao, haya masuala ya kulaza abiria kwenye viti vya airport ni ya kumalizwa mapema sana. Uendeshaji unahitaji mapinduzi .
 
Tunasubiri utekelezaji hapo. Zisije zikawa ni matamko tu kama ripoti ya CAG.
 
yataje kwa majina na hasara kiasi gani? ushauri wangu tuvunje board na kufuta kazi management tuwele zingine kwanza
Tangu enzi ya Nyerere hapajawahi kuwa na management ya Mswahili ikafanya vizuri hiyo ni ndoto.
Halafu usije ukadhani management nzuri inapatikana kwa kufanyisha interview wasomi wenye mavyeti mazito ni kazi bure,shida ni ukosefu wa uzalendo pamoja na uaminifu.
Hakuna ubunifu kila mtu anawaza kuiba bila kuangalia future wanawaza leo tu.
 
Air Tanzana haipo tena.... Ipo Air Zanzibar hivi sasa. 😆
 
lkn kama mashirika ya serikali yakishindwa wakuondolewa ni raisi kwa maana ndiye aliyeshindwa, raisi ndiye mkuu wa mashirika ya umma karibia yote hivyo kushindwa kunatokana na uongozi mbovu na incompetency upande wake …
 
Umeanza vizuri ila mwishoni umeharibu....Tanzania ni Tanzania na Pakistan ni Pakistan, sijui umeelewa.
 
Tanzania nadhani bado hatuja pata faida toka kwenye ndege zetu tulizo zinunua hivi karibuni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…