Msako wa Che Guevara: Jinsi gani Kikosi Maalumu toka USA kilihusika na mauaji ya Mwanapinduzi huyo

Msako wa Che Guevara: Jinsi gani Kikosi Maalumu toka USA kilihusika na mauaji ya Mwanapinduzi huyo

Nimeendeleza ingawa kwa kuufupisha kidogo kutokana na ufinyu wa muda na shughuli mbali mbali za ujenzi wa taifa. nashukuruni pia.
 
Nimeendeleza ingawa kwa kuufupisha kidogo kutokana na ufinyu wa muda na shughuli mbali mbali za ujenzi wa taifa. nashukuruni pia.
Uzi mzuri sana boss unauendeleza lini tujuze
Endeleza basi bro..
GuDume endeleza uzi huu wadau wako tunasubiri
aiseh umeniudhi kweli kukatisha hii story.umeniudhi sana.
Ndugu umejitahidi sana kuelezea hii Historia ya Che Guevara Big Up sana... But tatizo unataka kuiandika katika mfumo wa Riwaya wakati hii ni Historia. Nadhani ulitakiwa kuimalizia yote kabisa mpaka mwisho ili hadhira ipate elimu unayokusudia kuitoa. ingependeza sana
 
Ukisikia jina la Ernesto che guevera… kama wewe ni mhenga , msomi mzuri wa historia au mtu ambaye anapenda kujipatika elumu katika mambo mbalimbali hasa ya kisiasa akili yako haraka sana itakupeleka kwa jamaa mmoja ambaye kwenye picha anatokea akiwa na nywele shaghalabhala,ndevu na kofia. Ukimtizama utaona ni sura ya mtu aliye serious ingawa si sura ya kutisha. Ki rahis rahis utasema ni mtoto wa mama. Tahadhari : Cha Guevera hakuwa mtoto wa mama. Na usije ukajaribu kufikiria hivyo kwa kumtizama sura yake. utaumia.
View attachment 648609


Che guevera si kwamba anakumbukwa tu katika vitabu vya kihistoria kuwa alipata kuwepo lakini huyu anakumbukwa kama ni mmmoja ya watu ambao walikuwa kwenye blacklist ya US. Ambaye alikuja kuuawa na vikosi vya Bolivia ambavyo vilipata mafunzo toka marekani mwaka 1967 miaka 6 baada ya Uhuru wa Tanganyika. Mwa Argentina huyu ambaye ukimtizama unaweza mfananisha na ndugu zake wengine akina maradona. Lakini huyu yeye alikuwa na ufundi katika Nyanja nyingine kabisa miaka hiyo si kwenye kabumbu.

Aliamini katika siasa za Ki Marxist na alitaman kuona watu wanaishi katika usoshalist wa kimarx na katika hili aliamini kwa vitendo. Ni mtu ambaye kama ungemuuliza dini yake angekwambia kabisa yeye ni mfuasi wa Marx.


Kwa nini alikuwa tishio kwa jeshi la Marekani?


Che Guevera alikuwa mwanamapinduzi. Alikuwa mwanamapinduzi anayeishi kimapinduzi. Ambaye yeye hakuwa akiangalia rangi katika Imani yake,hakuwa akiangalia Dini au Races. Alikuwa anataka kuona dunia ambayo inaishi kisoshalist. Aliamini kuwa Uaa ilikuwa inahusika na matatizo mengi ya kiuchumi katika Dunia ya tatu hasa hasa amerika Kusini. Che akayatoa maisha yake kwenye uanamapinduzi. Kwanza akipigana bega kwa began na Fidel Castro kumwondoa aliyekuwa Dictator wa Cuba Fulgencio Batista mwishoni mwa mwaka 1950s na baadaye alijaribu kusambaza style ya kimapinduzi ya cuba afrika na amerika kusini.

Miaka kadhaa kabla ya kifo chake Che alikuwa ni kiumbe mwenye kuchukulika kama ana siri flani, hivi au wa kufikirika.kukiwa na minong’ono mingi kuhusiana na uwezo wake na namna ya ufanyaji kazi wake. Lakini kwa sasa ni wazi utamwona kwenye tshirts,vitambaa, vitabu na hata sinema kadhaa.

Nini kilimsukuma Che awe mwanamapinduzi?

Dhamira. Che alisukumwa na dhamira ya utu bora ,usawa kwa wote. Alikua akilelewa katika familia ya daraja la kati na kwenda shule ya udaktari. Maisha yake yalibadilika alipokuwa yeye na rafiki yake wakiwa katika safari ya kutumia pikipiki kukatisha amerika kusini mwaka 1952. Akipita nchi moja baada ya nyingine Che aliona watu Matajiri wakimiliki utajiri na wengi maskini wakipambana na hali zao katika umaskini wa kutupwa. Aliahidi angefanya jambo flani kutokana na hali hiyo. Kwa Che kuwa angefanya kitu alimaanisha kufanya Mapinduzi.

Akaanza kuwahubiria watu kuwa kakikundi ka watu wachache walio porini huko wakajifunza vizuri wanaweza kuondoa kwa haraka Serikali iliyo madarakani na kulikomboa Taifa. Miaka ya 1960 Wapiganaji wa Msituni walikuwa wanatishiwa na vita baridi katika ya Usoviet na Marekani. Mwaka huo US ilikuwa ikipigana Vietnam na mpaka mwaka 1967 Marekani ikazidi kupoteza ushawishi na umaarufu nchini mwake kutokana na majeruhi wengi katika vita vya Vietnam. Kukaanza kelele kwa nini wamarekani wakapigane huko.

Che akawa hatari Kijeshi alipoanza kuishambulia Bolivia. Kama alivyoelezea hapo baadaye alisema alitaka kuongezea Vietnam ya pili, ya tatu na kuendelea nyingi Zaidi katika Marekani kusini .


Ni namna gani Wamarekani walianza kumfuatilia.


Us walituma kwanza kikosi cha Kijani huko Bolivia ili kubadilisha waliokuwa wapiganaji wa kawaida wa Bolivia kuwa kikosi ambacho kingemsaka Che katika mapori au misitu ya Bolivia. Team ya Marekani ilikuwa ikiongozwa na Ralph “Pappy” Shelton ambaye ambaye alizaliwa Mississippi. Shelton aliacha shule akiwa grade 10 na akaamua kuwa katika mashamba ya katani akiokota katani na kufanya kazi mbalimbali huko ili kuisaidia familia yake. Akajiunga na jeshi mpaka kufikia hatua ya kuwa Meja.

Huyu bwana alipigana vita ya Korea ambako alijikumbia Medali nyingi sana na hivyo akapewa misheni hii ya mwisho huko Bolivia halafu baada ya hapo akatulie tu kula Bata. Hivyo Shelton akachagua watu wake pamoja nao akapita kununua Gita la kupiga Acoustic kwenye duka moja nje ya Fort Bragg, NC.

Sasa fikiria mtu mmoja mkakamavu Sana, mjeshi asiye na masikhara lakini unamwona akiwa analicharaza gitaa. Usingeweza kumdhania kwa ubaya… unajua. Tunajua mara nyingi wanajeshi wa aina yake ambayo kitaalam tunawaita decorated huwa ni watu mabangidu sana. So alikuwa akikaa na wanakijiji huku wakimsikiliza akicharaza gitaa lake la nyuzi sita.hii ilimfanya kuwa na ukaribu na wanakijiji.

Usiku Shelton angeanza kucharaza tena gitaa lake wanakijiji nao wakati mwingine wangekimbilia majumbani kwao kuchukua vifaa kadhaa vya muziki walivyo navyo kuja kujumuika naye na kuanza ku jam(kuburudika naye huko porini) walimwona ni mtu wa kawaida sana wakiburudika naye wakicheza na kuimba nyimbo mbalimbali. Baada ya hapo wanakijiji wakawa marafiki naye sana na kujikuta wanamwambia siri mbalimbali. Wakati huo huo yeye akiwaelekeza wengine kufuatilia zile informations alizokuwa akipewa na wanakijiji. Kama ambayo walimu wamekuwa wakifanya watu wa Shelton walikuwa wakiandaa lesson pal kila siku na kuwafundisha wanajeshi wa Bolivia.

mwendelezo...........

Basi wale askari waliopata mafunzo chini ya yule kamanda wa Kijeshi wa marekani wakapata taarifa toka kwa mkulima mmoja kuwa Che anaonekana maeneo flan. Kumbuka walishakuwa marafiki na wakawa kama jamaa zao tu. Hawa jamaa walipata mafunzo ndani ya miezi michache sana lakini walikuwa wameiva kama vile ni jeshi kamili. Yaani wenye uwezo.

Mpango ulikuwa ni kama ule uliowahi fanywa na kikosi maalum cha 7 huko Kolombia au mipango mbalimbali ambayo ilifanyika chini ya majeshi ya marekani huko Iraq na Afghanistan. Na nguvu hasa ya kikosi maalumu ilikuwa ni ni kufanya kazi pamoja na wakazi wa eneo husika. Walifanikiwa kwenda sehemu moja huko bondeni wanajeshi wa Bolivia waliokuwa wamepata mafunzo toka marekani na kumkuta mwanamapinduzi Che Guevera akiwa na wanajeshi wake wa msituni. Siku hiyo tarehe 8 oktoba walifanikiwa kukishinda kikosi alichokuwa nacho Che Guevera. Walimkamata Che na kumuua siku iliyofuatia yaani tarehe 9 oktoba. Kama ushahidi walimkata mikono yake na mwili wake ulizikwa kwenye kaburi ambalo halikuwa na alama yoyote kupoteza kabisa kumbukumbu yake (kama ambavyo ulifanywa mwili wa Osama kutupwa Baharini)

Mwaka 1997 mabaki ya Che Guevea yalipatikana na kutumwa kurudishwa Cuba ambako huko yalipata mazishi ya heshima yaliyoongozwa na aliyekuwa Rais wa Kipindi hicho wa Cuba Fidel Castro na kuhudhuliwa na waCuba wengi sana.

Huyu Che Guevera ni nani?

Ernesto Rafael Guevera De la Serna alizaliwa katika familia ya kitajiri ya kiargentina mwaka 1928. Akiwa anasoma udaktari (medicine) wa madawa au akisomea madawa katika chuo cha Buenos Aires siku moja aliamua kuzunguka Amerika Kusini kwa kutumia pikpik. Ndipo katik asafari hii alishuhudia umaskini uliokithiri na kunyanyaswa ,kukandamizwa kwa watu wenye kipato cha chini. Hivyo akapata kwanza Degree yake ya madawa mwaka 1953 na kuendelea na safari zake huko Latin America na kuanza kujihusisha na harakati za watu wenye mlengo wa kushoto. Ni miaka hiyo ya 1950s alipokutana na Fidel Castro. Kundi lake lilikuwa ni kundi lililopigwa marufuku huko Mexico. Ni Che aliyemsaidia fidel Castro kushika madaraka toka kwa aliyekuwa dikteta Fulgencio Batista mwaka 1959 na baadaye kufanya kazi kama mtu wa karibu sana wa Castro kama Waziri wa Viwanda. Che alikuwa akipinga kwa nguvu kabisa uwepo wa USA huko Latin Amerika. Castro anavyomwongelea Che husema huyu jamaa alikuwa “mtaalam wa vita vya kimapinduzi”

Guevara aliamua badaye kujiuzulu katik anafasi yake hiyo ya uwaziri. Inawezekana ni kutokana na tofauti zake na Fidel kuhusiana na Uchumi wa Taifa na sera za nje. Guevara akapotea Cuba na kusafiri kwenda Afrika na akaja tena kuonekana Bolivia ambako alikumbana na kifo chake. Kutoka hapo anakuwa ni mmoja ya watu wanaonekana kama mashujaa na wana mapinduzi akipingana na tawala za kibepari.

Hata hivyo si kila mtu anamwona Che kama shujaa.anashutumiwa kuhusiak vitu kadhaa ambavyo havikuwa vyema ikiwepo kuamuru mauaji ya mamia yaw a Cuba waliokuwa wamefungwa kipindi cha Mapinduzi.



Asanteni . Gudume Gwa Mbegu







Hapo nimekuelewa.ilikuwa nikulaani kabisa.
 
What??....GuDume Kutoka mambo na hadithi za papuchi hadi historia ya Guevara??[emoji53][emoji53][emoji53].....JF haiishiwi na maajabu!!
 
Back
Top Bottom