Msalaba wa Ajabu Kaburi la Kanumba

Msalaba wa Ajabu Kaburi la Kanumba

Ayo mambo watu wanaenda kufanya makusudi, na wengine ni wasanii wanahitaji wawe famous kama steven, kwa iyo wanatumwa na waganga wakafanye ivo vitu
 
Jambo limezua jambo! Baada ya hivi karibuni barua yenye ujumbe mzito kukutwa kaburini kwa aliyekuwa staa wa sinema za Bongo, marehemu Steven Kanumba, limezuka jipya ambapo kitu kilichopo kaburini kinachodaiwa ni msalaba (kilichozungushiwa duara pichani) kimemshangaza mama wa Kanumba, Flora Mtegoa.

Kitu hicho cha chuma chenye umbo la pembe tatu katikati kikiwa na alama ya msalaba, kwa juu kuna picha ya Kanumba, chini kuna maandishi ya DJ na katikati maandishi ya RIP SCK kilizua gumzo hivi karibuni kwenye kumbukumbu ya marehemu kutimiza miaka 4 ambapo baadhi ya watu waliohudhuria Makaburi ya Kinondoni alikozikwa walipigwa butwaa.
Baadhi yao walisema chuma hicho kilitengenezwa kwa mfano wa alama mojawapo ya imani ya Freemason ambayo baada ya kifo chake, kuna watu walihusisha kifo hicho na imani hiyo.

View attachment 338683 View attachment 338684 View attachment 338684

Msalaba wa ajabu wamshangaza mama Kanumba
Endapo kama ni kweli aliji husisha na imani hizo hakuna cha kushangaza hapo.
 
nami kesho napeleka ajabu langu mnitoe gazetini
 
Pole sana mama Kanumba, Kanumba alikufa kifo cha kijinga kabisa,lulu jamani tuambie kilichotokea ndani ya kile chumba,sipati picha Leo Kanumba angekuwa mbali sana,mama Kanumba angeshafika kula bata Hollywood,ToKEA Kanumba atutoke nilishaacha kuangalia kabisa movie za kibongo
 
kumbe jamaa alizaliwa mwaka 1977 na sio 1984 kama alivyokuwa akisema mwenyewe?!
 
DAAA! KANUMBAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA
 
Kanumba mbona yupo na anapiga dili zake hapa town kama kawa?
 
Mpaka pale ukweli wa Kilichotokea chumbani mpaka akafikwa na mauti then Marehemu atapumzika rasmi maana kadri anavyozidi kuzungumziwa na swali la "alikufaje" nalo linaibuka spontaneously. .........my opinion.
 
All those who have sold their soul to the devil and become members of secret
Society ni kawaida sana makaburi yao kuwekea hiyo pyramid ni kuonyesha kuwa alikuwa member.Lulu hana kosa pale katumika tu kama chambo,those demons he possessed ndiyo walimuuwa.
 
Back
Top Bottom