Msamaha wa Malimbikizo ya Riba ya Kodi ya Ardhi, Kuna Walakini Mahali

Msamaha wa Malimbikizo ya Riba ya Kodi ya Ardhi, Kuna Walakini Mahali

Lady Ra

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2014
Posts
879
Reaction score
991
Wakuu Kwema?

Mwezi uliopita niliona tangazo kutoka Waziri wa Ardhi, Mheshimiwa Angelina Mabula kua kama unadaiwa kodi ya Ardhi yenye malimbikizo ya riba juu yake basi ukilipa hiyo kodi utakua umesamehewa ile riba.

Mimi nina Kiwanja mkoa wa Kilimanjaro, na Kiwanja hiki kilitathminiwa kama cha biashara hivyo kodi yake ikawa kubwa. Sasa kuona hili tangazo nikaenda pale Halmashauri kuulizia kuhusu utaratibu wa kupata huo msamaha. Nilienda ili nifahamishwe katika deni langu kiasi gani ni deni la msingi na kiasi gani ni riba.

Nilichojibiwa ni kua huo msamaha ni tamko tu la Waziri lakini muongozo haujatoka bado. Nilijibiwa nilipe tu deni la ardhi lililopo sababu riba ni mpaka muongozo ukitoka pia msamaha utachukua muda kukubaliwa.

Nilijibiwa kua kwa system za Halmashauri zilivyo ni ngumu kupata "Statement" inayoonyesha deni la ardhi la kila mwaka, riba yake kila mwaka na kama kuna malipo yoyote yaliyofanyika toka deni lilipoanza mpaka kuonyesha balance ilivyopatikana.

Yaani ndo kusema kua msamaha huo hauwezekaniki sababu ni ngumu kujua unadaiwa nini na limetokea wapi. Sasa huu msamaha mtu unasamehewa lakini hujui ni kiasi gani umesamehewa ndio msamaha wa aina gani huu?

Maelezo haya nilipewa na mtu mkubwa tu pale Halmashauri kwenye Idara ya ardhi. Ina maana ye hajui au ndio utaratibu ulivyo?
 
Matamko mengi ya wanasiasa huwa yanakinzana na sheria na kanuni. Na mengine utekelezaji wake huwa na mlolongo mrefu...
 
Nahisi huyo aliyejibu hivo hakuwa na uelewa wa kutosha kwenye hilo swala, hiyo kitu ipo kweli nakushauri kama hukuridhishwa na majibu yake sogea ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Kilimanjaro ipo jengo la TRA mule Ndani utasaidiwa vizuri..
 
Wakuu Kwema?

Mwezi uliopita niliona tangazo kutoka Waziri wa Ardhi, Mheshimiwa Angelina Mabula kua kama unadaiwa kodi ya Ardhi yenye malimbikizo ya riba juu yake basi ukilipa hiyo kodi utakua umesamehewa ile riba.

Mimi nina Kiwanja mkoa wa Kilimanjaro, na Kiwanja hiki kilitathminiwa kama cha biashara hivyo kodi yake ikawa kubwa. Sasa kuona hili tangazo nikaenda pale Halmashauri kuulizia kuhusu utaratibu wa kupata huo msamaha. Nilienda ili nifahamishwe katika deni langu kiasi gani ni deni la msingi na kiasi gani ni riba.

Nilichojibiwa ni kua huo msamaha ni tamko tu la Waziri lakini muongozo haujatoka bado. Nilijibiwa nilipe tu deni la ardhi lililopo sababu riba ni mpaka muongozo ukitoka pia msamaha utachukua muda kukubaliwa.

Nilijibiwa kua kwa system za Halmashauri zilivyo ni ngumu kupata "Statement" inayoonyesha deni la ardhi la kila mwaka, riba yake kila mwaka na kama kuna malipo yoyote yaliyofanyika toka deni lilipoanza mpaka kuonyesha balance ilivyopatikana.

Yaani ndo kusema kua msamaha huo hauwezekaniki sababu ni ngumu kujua unadaiwa nini na limetokea wapi. Sasa huu msamaha mtu unasamehewa lakini hujui ni kiasi gani umesamehewa ndio msamaha wa aina gani huu?

Maelezo haya nilipewa na mtu mkubwa tu pale Halmashauri kwenye Idara ya ardhi. Ina maana ye hajui au ndio utaratibu ulivyo?

Karibu Tanzania ambako wazungu wanaugulia nyongo kutamani malipo kwa makampuni ya Simu yawe tozo za serikali.
 
Matamko mengi ya wanasiasa huwa yanakinzana na sheria na kanuni. Na mengine utekelezaji wake huwa na mlolongo mrefu...
Sasa wametoa matamko lakini sidhani kama wamewaelewesha watendaji wao vilivyo juu ya huu msamaha. Matokeo yake watendaji hatuwaelewi. Au inaweza kua pia watendaji wanaelewa ila ndio hivyo tena kila mtu anakula ofisini kwake na mkono mtupu haulambwi.
 
Nahisi huyo aliyejibu hivo hakuwa na uelewa wa kutosha kwenye hilo swala, hiyo kitu ipo kweli nakushauri kama hukuridhishwa na majibu yake sogea ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Kilimanjaro ipo jengo la TRA mule Ndani utasaidiwa vizuri..
Ahsante kaka yangu,
Nitajaribu kwenda hapo. Shida yangu ni kupata kwanza statement ambayo iko "itemized".
 
Back
Top Bottom