MSAMBARATIKO: Baadhi ya maeneo nchini yajipanga kujitangaza jamhuri kisa uchaguzi

MSAMBARATIKO: Baadhi ya maeneo nchini yajipanga kujitangaza jamhuri kisa uchaguzi

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Habari zenu familia ya JF. Kwa mujibu wa Redio DW ya Ujerumani idhaa ya kiswahili Leo mchana, wametangaza huenda taifa imara kiuchumi Africa Mashariki yaani Kenya huenda likagawanyika kisa uchaguzi wa hivi majuzi.

Tangazo hili la kugawa baadhi ya maeneo na kuwa nchi ama jamhuri limetolewa na mmoja wa washauri wa muungano wa Upinzani NASA aliyekaribu na Raila Odinga.

Ikumbukwe kuwa kuna kesi mahakamani ikilalamikia ushindi wa Uhuru Kenyatta. Hata hivyo eneo au maeneo yanayojipanga kujitenga hayajatajwa bado. Kenya imegawanyika kikabila huku uhasama wa kihistoria wa kikabila ukikita mizizi. Makabila makubwa ni wakikuyu, wakalenjin, wajaluo, waluya, wakamba na wamasai.
========

Mshauri wa kiuchumi wa Muungano wa upinzani NASA, David Ndii, ameibua mjadala mkali baada ya kusema katika mahojiano ya televisheni kuwa wakati umewadia kwa sehemu nyengine za Kenya kujitenga.

Mwanasheria Mkuu wa Kenya, Githu Muigai, amekemea vikali maoni hayo akisema yataligawa taifa hata zaidi kwa misingi ya kikabila. Caro Robi amezungumza na mchambuzi wa masuala ya kisiasa, Herman Manyora, na kwanza amemuuliza mtizamo wake kuhusu suala hilo la baadhi ya maeneo kujitenga ili kujitawala.

CHANZO: DW
 
Wavumiliane watafika tu.. utengano unamadhara makubwa sana.. Angalien Sudan Kusini wanavyouana wenyewe na kuteseka na njaaa
 
Hawa inatakiwa sasa uongozi uende kwa rotation kikabila otherwise wapigane vita wauane haswa hapo ndipo watakapoheshimiana
Mbona kwenu mlikataa rotation na zanji?.au unadhani wao walikuwa hawautaki huo usukani?.
 
  • Thanks
Reactions: 999
Wakikuyu (Kenyatta) wameunganisha nguvu na wakalenjini ( William Ruto) kuhakikisha wanatawala mpaka mwisho wa dunia! Hapo hakuna namna! Ndiyo makabila makubwa zaidi Kenya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona kwenu mlikataa rotation na zanji?.au unadhani wao walikuwa hawautaki huo usukani?.
Sisi hatuna hiyo kitu bongo tunaheshim sana utawala wa sheria na katiba.. ndio maana unaweza kuona rais akitoka bara makam n mzenji na vice vesa iz tru
 
Kuna kitu kinasikitisha aisee: yaani unasikia watu wakisema wazi kuwa urais wa nchi ni kwa kikuyu na karenjin tu huku ukiano akina saitoti, Kaisery, Ouko nk wakipotea katika mazingira tata. Pia hata Msando akisema atahakikisha system inatoa matokeo bila chenga anauawa tena kwa dhiaka ya kukata kidole alichosema ndio password.
Mungu apishe mbali.
 
Mbona kwenu mlikataa rotation na zanji?.au unadhani wao walikuwa hawautaki huo usukani?.
Walikuwa wanautaka uongozi sana sasa hawa waliokalia kiti nao hawataki kuachia.
Hata pale Zanzibar yatakuja kuwa hivi hivi kama huko.
Kugawanyika kuko wazi kabisa either Zanzibar ijitenge na bara au Pemba ijitenge na Unguja
 
Wakikuyu (Kenyatta) wameunganisha nguvu na wakalenjini ( William Ruto) kuhakikisha wanatawala mpaka mwisho wa dunia! Hapo hakuna namna! Ndiyo makabila makubwa zaidi Kenya.

Sent using Jamii Forums mobile app
I feel an anguish when I read these hatred tribal stories in Kenya and other places! Stop this nonsense, you people.
 
Haya mambo yalitakiwa kujadikiwa mara tu walipo pata uhuru. Lakini viongozi wa wakati huo waliogopa kuligusa hili swala kwasababu kama hizi hapo juu (utengano). Pili waliogopa kuligusa kwasababu zao binafsi ambazo ni mali walizozishikilia zingepotea kama nchi ingejigawa na kuwa mataifa madogo tofauti. Kinacho hitajika hivi sasa ni busara na kupunguza tamaa ya kwa baadhi ya viongozi.
 
Back
Top Bottom