Msameheni bure Job Ndugai, amechanganyikiwa baada ya kuomba msamaha batilifu uliokataliwa! Barua yake ya Kujiuzulu nayo pia ni batilifu!

Barua ya kiofisi kwanini iandikwe capital letters,
Pia why atumie headed paper ya bunge kwa barua binafsi.

Tusaidie, nimeona as if he signed kwa kalamu ya kijani, hiyo ni kwa matumizi ya kiofisi kwa ngazi fulani.

Even if ameandika hii barua alikuwa hatatulia, au tuseme alikuwa under pressure kubwa.
 
M
Munatutisha bandugu ??!!!
 
Haitakuja kutokea kwa mwana mageuzi akamsamehe Ndugayi hata siku moja.

Ametunyanyasa sana kwa kiburi na jeuri ya Jiwe na hili jambo liwe ni fundisho kwa wanao baki kuwa mwenye kuhukumu ni Mungu tu.
 
Mkuu Paschal , hongera kwa uchambuzi mzuri, Mimi nakubaliana na wote wanaosema hii si barua ya Ndungai ya kujiuzulu. Hii ni taarifa kwa umma, maana yake ni kwamba, baada ya Ndungai kuandika barua ya kujiuzulu, akaandika na hii- ili kuurarifu umma. Lakini pia tuna la kujifunza kutokana na tukio zima la Ndungai , hasa tukirejea kwenye rasimu ya katiba ya Mzee Warioba- kwamba Kuna baadhi ya nafasi za uongozi, ikiwemo na usipika- wagombea wawe huru, wasitokane na vyama.
 
Binafsi ninaamini hii barua hakuandika Ndugai, huenda imeandikwa na maUVCCM yaliyojazana pale TISS. Kifupi huenda Ndugai hakuwa tayari kujiuzuru lakini akalazimishwa na mamlaka kujiuzuru.

Yote kwa yote Ndugai hakuwahi kuwa mtu mwenye kufuata kanuni na kutenda haki pale bungeni, hata haya ya kujiuzuru kihuni ni mwendelezo ule ule wa kihuni.
 
Kwa Mara ya Kwanza Pascal umenifuraisha, Kuna muhimili 3 Bunge, Mahakama na Serikali. Muhimili wa Bunge kazi yake ni kusimamia Serikali sasa Kama Spika anadhalilishwa hivi maana hatuna mihimili 3 Bali muhimili 1.
 
Ni cheo cha bunge alichokipata kwa njia ipi?!

Na ataanzaje kupeleka kwa mamlaka ya kibunge kabla hajawajuza waliomtuma?!

Na ingawaje Ibara ya 149 (1)(c) inamtaka Spika kuwasilisha TAARIFA bungeni pale anapojiuzulu, hizo ni protocol za kiofisi tu lakini hawezi kujiuzulu bila kuiarifu mamlaka iliyomtaka akagombee uspika!! Ni kama Rais tu, nae akijiuzulu, Ibara ya 149 (1)(b) inamtaka awasilishe TAARIFA kwa Spika, nazo ni protokali za kiofisi tu lakini hawezi kufanya hivyo bila kumwandikia kwanza Katibu wa Chama Chake!!

Neno taarifa nimeliweka kwa msisitizo kwa sababu tulichokiona sisi sio Barua ya Kujiuzulu bali taarifa ya kujiuzulu! Barua ya kujiuzulu ilienda kwa waliomtuma agombee uspika, nao wakapeleka nakala kwa Katibu wa Bunge ambae nae akatoa TAARIFA kwa umma!
 
Kwani ni mangapi Ndugai aliyafanya ndani ya Bunge pasipo kufuata utaratibu? Ndugai sio sio muumini wa kufuata katiba yeye ni mtu wa Maguvu na sifa.
Nampongeza sana Mh. Rais kwa kuukataa msamaha ule batili wa Ndugai
 
Umenikumbusha Luca Brasi, it's either your signature or your brain will be on the paper.
 
Punguza sauti 😁😁😁😁
 
Mkuu wala usipate taabu na hawa watu. CCM ilishaharibu taratibu zote za Nchi. Hakuna kufuata Katiba wala Sheria za Nchi. Nchi imekuwa ikiendeshwa Kwa matamko. Ni hatari Sana. Katiba Mpya ni muhimu mno, vinginevyo tutaangamizwa na hawa watu wenye uroho wa madaraka.

Hebu fikiria Wabunge wanaacha kuungana na Mkuu wa Mhimili wao unaojitegemea wanaungana na Mkuu wa Mhimili mwingine wa Serikali, kisa ni Mwenyekiti wa Chama Chao.

Je ni lini basi Bunge litasimamia na kuishauri Serikali??? Suala la Ndugai limebeba uzito mkubwa sana dhidi ya Katiba yetu ya sasa.
 
Hiyo sio barua ya kujiuzulu ni barua ya kutoa taarifa kuwa ameandika barua ya kujiuzulu, tunasubiri barua yenyewe ya kujiuzulu ameandikaje maana hiyo bado haijawekwa hadharani.
 
Paskali usitupotezee muda wa kusheherekea kujiuzulu kwa huyu mgogo,
Barua iwe imekua adresses CCM,CHADEMA,ACT, NCCR haitusaidii kwa sasa cha msingi mpuuzi yule kaachia ngazi.


OVER
 
Hii sio barua ya kujiuzulu ni taarifa kwa vyombo vya habari tu. Barua atakuwa kapeleka kwa wahusika. so relax Bwana Paskali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…